Monday, January 1, 2018

Lema apewa tahadhari na Humphrey Polepole




Katibu wa Itikadi na Uenezi  wa  Chama Cha Mapinduzi CCM, Humphrey Polepole amemtahadharisha Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema kwakumwambia kuwa  kipindi hiki ni cha mwisho kuongoza Jimbo hilo la Arusha Mjini.

Hoja hiyo ya Polepole kumtahadharisha Mbunge huyo wa Arusha Mjini (CHADEMA)  inakuja baada ya Mbunge huyo kupitia kurasa zao za twitter wajikibizana huku Lema akionyesha kumhoji Polepole kama familia yake huwa inamuelewa kweli?

Kupitia ukurasa wake wa twitter “Term ya mwisho Arusha, tunataka Mbunge wa Masuala na si wa Matukio, hata mkichezesha draft ili uende Hai, haitawezekana maana hata "fly to..." maji yako shingoni, na ukiamua kurudia kazi ya "zamani" anko Siro is very serious.,” ameandika Humphrey Polepole.



No comments:

Post a Comment