Saturday, January 13, 2018

JAMANI ANTIII…NISHUSHE UNUNIO-11


ILIPOISHIA KWENYE RISASI JUMAMOSI:
“Unajua Mungu anatuvumilia kwa mengi sana, mama yangu vile, wewe niamini mimi,” Bigambo alikomelea maneno hayo yasiyofaa na kusikilizika kwa mtu mwenye akili timamu isipokuwa mlevi tu mwenye kuzidiwa na kimea kikali.

“Kweli eeh, unajua kila nikikuangalia nakutafakari sana na kuona kama wewe siyo binadamu wa kawaida, yaani nakuona kama kiumbe cha ajabu au mtu aliyewahi kuzaliwa, akafa na kufufuka tena, yaani unaishi kwa mara ya pili,” Vivian naye alijibu maneno ambayo waliokuwa wamekaa meza ya jirani kwakinywa maji na soda walianza kucheka kufuatia maneno ya Vivian kutoka kwa mpangilio usioeleweka.

Wakati wakiendelea kunywa, ghfla kuna mtu alisimama mbele yao na kumshika Vivian bega na kumuuliza alikuwa akifanya nini hapo na aliyekuwa amekaa naye ni nani kwake? Mkononi alikuwa na kitu kilichowashtua wote wawili.
SINDIKIZANA NAYO HAPA CHINI…
VIVIAN aliamka kabisa na kubaki ameshika kiti kwa mkono mmoja. Midomo ikimtetemeka kwa hasira isiyosimulika. Mtu aliyekuwa amesimama mbele yao alikuwa ni Jisu, yule fundi aliyemtengeneza mlango siku ya ugomvi wake na mzazi mwenzake, na mwisho wa siku wakaishia kushiriki dhambi tamu kutokana na kuzidiwa na kushawishiwa na vimea vya Reds na Nyagi.

Mkononi mwa Jisu kulikuwa na mzinga mkubwa wa nyagi, tena ikiwa haijafunguliwa lakini kwa macho ya harakaharaka ni kwamba Jisu alikuwa chakari kwa ulevi kwani hata ongea yake iliashiria jambo hilo kwa uwazi kabisa na pia hakuacha kuyumba na kujiweka sawa kila mara, alikuwa twiiiii, kama siyo bwiiiiiii achilia mbali bwaksiiiiii, maisha ya mitungi yana raha na karaha zake jamani.


No comments:

Post a Comment