Saturday, January 13, 2018

Video | Mr Nana – Tanga Ya Leo | Mp4 Download

Video | Mr Nana – Tanga Ya Leo | Mp4 Download

Video | Mr Nana – Tanga Ya Leo | Mp4 Download


DOWNLOAD

Audio | Mr Nana – Tanga Ya Leo | Mp3 Download

Audio | Mr Nana – Tanga Ya Leo | Mp3 Download

Audio | Mr Nana – Tanga Ya Leo | Mp3 Download
DOWNLOAD

JAMANI ANTIII…NISHUSHE UNUNIO-10



ILIPOISHIA KWENYE RISASI JUMAMOSI:
Kwere aliondoka na kumuacha Bigambo akiwaza hili na lile kichwani mwake juu ya namna gani aanze kuishi na wale watu wa ofisini kwake. Ni kweli waliwahi kumuumiza kwa mambo mengi sana lakini kwa hili lilikuwa pigo kubwa kwani kumsemea kwa meneja kwamba ana uhusiano usiofaa na Vivian ilikuwa ni kumharibia kwa sehemu zote mbili. Kwamba anaweza kutimuliwa kazi na kumkosa Vivian ambaye alikuwa amemuonjesha penzi tamu kuwahi kupewa tangu aanze kujihusisha na masuala hayo.
Wakati Bigambo akiwazua hayo, ghafla simu yake iliita na alipoitazama kwenye kioo, ilikuwa namba ngeni na akaipokea harakaharaka na kuiweka sikioni huku akisikilizia ni nani alikuwa amempigia na alikuwa na ishu gani.
Mpigaji wa simu ile alikuwa Vivian, aliamua kumpigia kwa namba ngeni akiwa na maana kubwa sana.
“Enhe, imekuwa hivyo tena? Ayaa kwa nini Vivian? Yeye amekuambiaje?” Bigambo aliuliza kwa hamaki baada ya kuambiwa maneno f’lani na Vivian yaliyochoma moyo wake kwa ncha kali ya kisu chenye moto mkali.
SHUKA NAYO SASA…
BIGAMBO alihamaki mno. Maneno ya Vivian yalikuwa yamemuondoa kabisa kwenye mudi ya kufanya chochote. Alichokifanya ni kuzungumza na mmoja wa viongozi wake na kumuomba ruhusa ya kwenda nyumbani kupumzika akisingizia kichwa kinamuuma ingawa ukweli ni kwamba alikuwa na msongo mkubwa wa mawazo.
***
Baada ya kutoka kwa meneja, Vivian alikuwa amechanganyikiwa kupindukia. Tangu aanze kujihusisha na masuala ya mapenzi, hakuwahi kufikishwa kwa kiongozi wake wa kazi hata kabla ya kuanza kufanya kazi hapo. Aliifikiria aibu atakayokumbana nayo pale ofisini endapo suala la kuitwa kwa meneja litawafikia wafanyakazi wenzake.
“Lazima nifanye uamuzi mkubwa bila kujali utamuumiza nani na kwa kiwango gani, lazima niachane na Bigambo na sitaki tena kujihusisha na mapenzi na mfanyakazi mwenzangu kuanzia leo,” Vivian aliwaza huku akishika simu yake na kumpigia Bigambo kwa namba ambayo hakuwahi kumpigia nayo na kumueleza ukweli ambao alitarajia kukutana na lawama lakini hakujali sana kwani alikuwa ameamua kutoka moyoni kwamba ni lazima aachane na Bigambo.
Bigambo aliondoka akiwa na mawazo mengi kichwani mwake. Hakujua ataishije bila Vivian licha ya kwamba walikuwa na muda mfupi sana tangu wafahamiane na kupeana penzi mara moja, lakini mahaba ya mwanamke huyo kutoka Tanga yalimkolea sana kijana wa watu.
“Nitaishije mimi bila huyu mwanamke? Mimi ni kidume, nitambembeleza kwa kila njia kuhakikisha namuweka sawa tena kwenye himaya yangu, siwezi kuruhusu kirahisi hivi aniache, siwezi hata kidogo,” Bigambo naye alipangilia mawazo kichwani huku akidandia daladala, tayari kwenda nyumbani kujilaza ili apunguze mawazo.
Alilala hadi mchana ambapo aliwasha simu yake aliyokuwa ameizima tangu afike nyumbani. Meseji zilianza kumiminika moja baada ya nyingine kutoka kwenye mtandao ukimjulisha namba ambazo zilikuwa zimempigia akiwa amezima simu, namba ya Vivian ilikuwa miongoni mwa namba hizo.
“Mmmh,” Bigambo aliguna kwanza huku akishindwa kuamini kama ni kweli Vivian alikuwa amempigia tena licha ya kumwambia maneno ya kuachana tena kwa sauti kavu isiyokuwa na masihara hata chembe.
“Amenipigia kweli? Anataka kuniambia nini zaidi ya kuniumiza zaidi? Ngoja nimpigie nisikie tena anachotaka kuniambia lakini kama ni yaleyale ya kusisitiza kwamba ameachana na mimi sitampa nafasi ya kumsikiliza, sitaki maumivu tena nikiwa najiandaa kumrejesha, Bigambo aliwaza moyoni na kumpigia Vivian ambapo alikuta namba ikiwa inatumika, hivyo alilazimika kusubiri kwa muda.
Aliagiza chakula na wakati ananawa, simu yake iliita na alipoitazama aliona jina la My Vivian, kama alivyokuwa amelihifadhi kwenye orodha ya majina yake ya simu. Moyo ulimlipuka na kujikaza kiume ambapo aliipokea simu kwa nidhamu zote akijiandaa kusikia lolote kutoka kwa mwanamke huyo mrembo.
“Salama kabisa, nakusikiliza Vivian,” Bigambo aliharakisha ili kujua lengo la Vivian kumpigia tena simu.
“Nilikuwa nimelala ndiyo maana nikazima simu.”
Licha ya kujiapiza kwa dhamira ya kweli kwamba hataki tena mapenzi na mtu wa ofisini, moyo wa Vivian ulikuwa bado na hisia za kimapenzi kwa Bigambo, mwanaume ambaye alimuonesha upendo wa kweli kabisa na hata kwenye uwanja wa fundi seremala, alikuwa akijiweza vilivyo.
“Hapana, zilikuwa ni hasira hizo, naomba tuonane tuzungumze tena ili tuone tunafanyaje, tafadhali naomba my love, nakupenda sana Bigambo nimeulizia nikaambiwa umeomba ruhusa ya kwenda nyumbani kwa kuwa unaumwa kichwa, naomba nije nikuone mpenzi wangu, nakuja sasa hivi nikifika hapo Riverside nitakupigia unielekeze nyumbani kwako,” Vivian alisema mfululizo bila kumpa Bigambo nafasi ya kusema chochote na kisha kukata simu, jambo ambalo lilimuacha njia panda kijana wa watu.
“Duh! Huyu demu kiboko aisee, mbona hii ni ajabu sana? Yaani ametoka kunitamkia maneno makali muda siyo mrefu akinitaka niachane naye halafu sasa hivi anataka tuzungumze tena na anadai ananipenda sana, mapenzi ni kitu cha ajabu sana jamani,” Bigambo alijisemea moyoni huku akifurahi kimyakimya.
Dakika 45 baadaye, simu ya Bigambo iliita tena na alipoitazama mpigaji alikuwa ni Vivian, akatabasamu na kuipokea haraka sana.
“Umefika? Basi njoo hadi pale pa siku ile nitakufuata nikupeleke nyumbani,” Bigambo alijibu na kuanza kujisogeza kwenye ile baa waliyokaa na Vivian kwa mara ya kwanza walipokutana kwa ajili ya mazungumzo na kuishia kufanya kweli.
Vivian alitembea kwa haraka, moyoni akiwa na shauku ya kumuona tena Bigambo. Nafsi ilikiri kabisa kwamba alimpenda mno mwanaume huyo, ingawa walikuwa na muda mfupi tangu wakutane. Muda mfupi alifika na kumfahamisha Bigambo ambaye alifika na kumchukua hadi nyumbani kwake.
“Pole kwa kuumwa na kichwa baba,” Vivian alianza mazungumzo kwa maneno hayo huku akimshika kichwani Bigambo, ambaye alibaki ametulia kimya bila kupinga chochote.
“Lakini Vivian, mbona umeniumiza sana moyo leo, ni kwa nini uliamua kunieleza maneno makali namna hiyo?” Bigambo naye alijibaraguza ingawa moyoni alifurahia sana kitendo cha Vivian kumtafuta na hatimaye kukaa pamoja, tena ikiwa chumbani kwake.
“Tuachane na hayo baba, ndiyo maana nimekuja tuyamalize, unajua maneno ya meneja yalinichanganya sana na kujikuta nikijawa na hasira kali lakini baada ya kutafakari kwa kina nimegundua kwamba nakupenda sana mpenzi wangu na kamwe siwezi kuishi bila penzi lako, nisamehe kwa kukuumiza baba yangu, sitarudia kweli tena,” Vivian alisema huku akimpapasa Bigambo kichwani na kuyachezea masikio kwa kuyaminyaminya na kuyakanda, kitendo kilichoanza kuamsha hisia za mambo f’lani kwa Bigambo.
“Sawa, nimekuelewa lakini siku nyingine tusiumizane hivi bwana, sawa mama?” Bigambo alisema ingawa sauti yake ilitoka kwa tabu kutokana na kuanza kuelemewa na mahaba mazito.
Ili kutoonekana goigoi au mshamba wa mambo hayo, Bigambo naye alianza kujibu mashambulizi kwa Vivian. Alipeleka mkono wa kulia shavuni kwa Vivian na kuanza kupapasa taratibu lakini hakuishia hapo na badala yake alihamishia kiganja shingoni na kuwa kama anacharaza gitaa, kufikia hapo Vivian akaanza kufumba na kufumbua macho kwa tabu kama anayenyemelewa na usingizi mzito.
“Oooh, baba jamani,” Vivian alianza kulalamika na kujikunjakunja huku naye akiendelea na zoezi la kupashana joto. Ilifika mahali mpambano ulikolea na kwa pamoja wakajikuta wakiwa hoi na kilichoendelea kilimtosha kila mmoja wao.
Mtanange aliouonesha Bigambo kwa Vivian haukuwa wa nchi hii. Alifanya kwa makusudi ili arejeshe adabu na kweli alifanikiwa kwani alifanya kwa kiwango ambacho hata yeye alishangaa mno.
Baadaye walipitiwa na usingizi mzito ambapo walishtuka ikiwa ni saa mbili kasoro dakika kadhaa usiku. Bigambo akitarajia baada ya kukurupuka, Vivian angeanza harakati za kuondoka, lakini ndiyo kwanza mama wa watu akaendelea kujilaza huku akijibaraguza kwa maneno yasiyokuwa na msingi wowote.
“Niambie my love,” Vivian alisema huku akimshika Bigambo kichwani na kuzichezea nywele ambazo zilikuwa zinaanza kuota kwa mbali.
“Nakusikiliza mama yangu,” Bigambo alijibu akitarajia kusikia neno la ‘nataka kuondoka’ kutoka mdomoni kwa Vivian, lakini alichokisikia ni kingine kabisa.
“Tunakula nini usiku huu kabla ya kulala mume wangu?’ Vivian aliuliza swali ambalo Bigambo hakulitarajia kabisa na kujikuta akitabasamu.
“Wewe unataka tule nini?” Bigambo naye alimuuliza.
“Nakusikiliza wewe baba.”
“Kwani unalala hapa?” Bigambo aliamua kutoa dukuduku lake.
“Ndiyo mume wangu au hupendi nilale na wewe jamani, sema basi niondoke?” Vivian alisema na kuinuka kabla ya kukaa sawa kitandani na kumtazama Bigambo kwa jicho la kusikilizia jibu lake.
Kabla Bigambo hajajibu chochote, ilisikika sauti ya jirani wao ikimuita Bigambo.
“Wewe Bigambo wewe?”
“Naam.”
“Njoo kuna mgeni huku nje.”
“Ni nani huyo?”
“Wifi amekuja,” sauti ya nje ilisikika na hapohapo Vivian akamtazama Bigambo kwa hamaki huku akishindwa kuamini alichokisikia.
Je, ni wifi gani tena huyo? Usikose kufuatilia siku ya Jumamosi kwenye Gazeti la Risasi. 0673 42 38 45.
NA IRENE MWAMFUPE NDAUKA

SEVEN DAYS IN HELL (SIKU SABA KUZIMU)- 48


ILIPOISHIA:
“Nakupenda Jamal,” alisema kisha akanibusu kwenye shavu langu la upande wa kushoto, mwili wote ukasisimka tena, nikakosa hata cha kujibu zaidi ya mimi kumkumbatia pia na kumbusu, uvuguvugu wa joto la mwili wake ukanifanya nitamani niendelee kumkumbatia lakini nilipokumbuka mtihani mzito uliokuwa mbele yangu, nilimuachia, nikatoka haraka na kwenda kumuamsha Raya, harakaharaka tukaanza kujiandaa.
SASA ENDELEA…
Muda mfupi baadaye, tayari tulikuwa tumeshamaliza kujiandaa, mimi na Raya tukasaidiana kumbeba Shenaiza ambaye bado alikuwa haelewi chochote kinachoendelea, Firyaal akaenda kuwasha gari. Ilibidi kila kitu kifanyike harakaharaka kama Shamila alivyotuambia.
Kwa bahati nzuri tulifanikiwa kutoka salama, tukafunga milango yote na kuiacha funguo mahali alipokuwa ametuelekeza Shamila. Kwa kuwa bado ilikuwa ni asubuhi, hakukuwa na foleni sana barabarani, safari ya kuelekea Kimara Temboni ikaanza.
Ilibidi nimuombe Raya simu yake kwa ajili ya kumpigia yule mtu ambaye Shamila aliniambia kwamba ni ndugu yake ambaye ndiye angeenda kutupokea na kutupa hifadhi. Namshukuru Mungu kwamba nilivyopiga mara moja tu, alipokea, tukazungumza na kuelewana.
Nikawa namuelekeza Firyaal kama na mimi nilivyoelekezwa na yule mwenyeji wetu, kwa bahati nzuri tulipofika Kimara Temboni tu, mwanamke wa makamo, mweupe na mnene kiasi, alitupokea. Yeye alikuwa amepanda bodaboda, akatonesha ishara kwamba tumfuate, Firyaal ambaye alikuwa na uzoefu wa kutosha wa kuendesha gari, akawa anamfuata.
Tulishuka makorongo mpaka tulipotokea ng’ambo ya pili, akasimama mbele ya geti kubwa jeusi na kumlipa yule dereva wa bodaboda, akasubiri mpaka aondoke kisha ndiyo akatufuata. Kwa kuwa kiumri alikua mkubwa kwetu, sote tulimuamkia kwa heshima, akamwambia Firyaal inabidi aliingize gari ndani ya geti kwa usalama zaidi.
Akatufungulia geti na muda mfupi baadaye, tayari tulikuwa ndani, tukasaidiana kumshusha Shenaiza mpaka ndani, akatukaribisha na kututaka kuwa makini kwa muda wote ambao tutakuwa pale nyumbani kwake.
“Inaonesha mambo siyo mazuri kwa Shamila, nimetoka kuongea naye sasa hivi na yeye ndiye mtuhumiwa namba moja, lazima atapewa kashikashi kubwa na polisi kwa hiyo inabidi sote tutulie tusije tukasababisha matatizo mengine, kuweni makini sana na simu zenu,” alisema, wote tukatingisha vichwa kama ishara ya kumuelewa.
Kwa kuwa nyumba ilikuwa kubwa, alitupangia kila mmoja chumba chake na kutuambia tutakaa hapo mpaka mambo yatakapotulia. Ilionesha kwamba mwanamke yule anajimudu sana kimaisha kwa jinsi mazingira ya pale nyumbani kwake yalivyokuwa.
Muda ulizidi kuyoyoma huku nikiwa na shauku kubwa ya kutaka kujua nini kitatokea kwa Shamila kwani kama ni matatizo, basi tulikuwa tumemsababishia makubwa sana.
“Kuna anayejua kufanya ‘meditation’ kati yenu?” aliuliza mwanamke huyo ambaye baadaye alituambia kuwa tuwe tunamuita mama wawili, wote tukatazamana.
“Shamila yupo kwenye matatizo makubwa, inatakiwa tufanye kitu kumuokoa vinginevyo mambo yatakuwa mabaya sana kwake,” alisema, nikashindwa kuelewa uhusiano uliokuwepo kati ya kufanya meditation na kila alichokuwa anakizungumza.
“Kwani meditation ni nini?” nilimuuliza nikiwa na shauku kubwa, akanitazama bila kunijibu chochote kwa sekunde kadhaa kisha atatuambia mimi, Raya na Firyaal tumfuate, tukaingia ndani ya chumba kimoja kilichokuwa kimetandikwa zulia jekundu la bei mbaya.
“Hata kama hamjui ni lazima tushirikiane kumsaidia Shamila, mimi peke yangu siwezi, nitawafundisha nini cha kufanya,” alisema, sote tukashusha pumzi ndefu na kuanza kumsikiliza. Akatuambia kwamba kwa kawaida, binadamu tuna nguvu kubwa zisizoonekaa kwa macho, ambazo kama zikitumiwa vizuri zinaweza kutoa matokeo makubwa.
Akasema jukumu la kwanza ambalo tulitakiwa kulifanya kwa muda huo, ilikuwa ni kumkomboa Shamila kutoka kwenye mkono wa sheria, sikumuelewa kabisa alichokuwa anamaanisha, ikabidi nimuulize.
Akaniambia kwamba tunatakiwa wote tukae na kutulia katika mkao ambao kila mmoja wetu ataruhusu nguvu aliyonayo itumike kwa ajili ya kazi iliyokuwa mbele yetu, bado sikumuelewa zaidi ya kuona kama ananichanganya kichwa.
“Kuna kitu kinaitwa out of body experience au kwa kifupi OBE, yaani mwili wako unakuwa upo hapa lakini kwa wakati huohuo unakuwa sehemu nyingine tofauti ukifanya kitu kingine tofauti kabisa,” alizidi kutueleza lakini bado kwangu ulikuwa ni sawa na usiku wa giza.
Hamjawahi kusikia au kuona mtu anajitazama mwili wake mwenyewe akiwa nje ya mwili huo?” alisema kitu ambacho kiliushtua sana moyo wangu, mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio. Kilichofanya nishtuke ni kwamba kile alichokuwa akikizungumza, mimi kilishawahi kunitokea lakini nilikuwa sijui ni nini na inakuwaje.
Nilikumbuka vizuri siku nilipovamiwa na wale watu ambao walinishambulia vibaya na kutaka kuyakatisha maisha yangu, muda huohuo nikaanza kuhisi kama napaa halafu nikawa nauona mwili wangu ukiwa umelala chini, damu nyingi zikitoka kwenye jeraha la kifuani.
Nilikumbuka kila kitu ambacho kiliendelea kutokea na maruweruwe yote mpaka siku nilipokuja kuzinduka na kurejewa na fahamu zangu.
“Mbona kama uko mbali kimawazo? Tunaenda pamoja kweli?” alihoji mama wawili huku akiwa amenikodolea macho, nikawa namtazama lakini akili zangu zipo kwenye ulimwengu mwingine kabisa, ni kama alijua kwani alinishika na kusababisha nishtuke sana, wote wakawa wananishangaa.
“Ili hiki tunachoenda kukifanya kitimie lazima kila mmoja akili zake ziwe hapa, umenisikia kaka?” alisema mama wawili akinilenga mimi, nikashusha pumzi ndefu na kukaa vizuri. Akaendelea:
“Sasa kwa kuwa kati yenu hakuna anayejua tunachoenda kukifanya, nawaomba kila mmoja atulie tukiwa tumeshikana kisha mimi nitazitumia nguvu zenu kufanikisha hili linalotukabili, mambo mengine tutaendelea kuelekezana taratibu, tumeelewana?” alisema, wote tukaitikia kwamba tumemuelewa.
Akatuelekeza namna ya kukaa, wote tukakunja miguu na kuzunguka kama duara, akatuambia kila mmoja anatakiwa afumbe macho, ainue shingo yake na kupumua kwa uhuru kabisa huku akitutaka kutuliza akili zetu sehemu moja.
“Unatulizaje akili sehemu moja?”
“Nyie wote si mnaijua vizuri hospitali anayofanya kazi Shamila si ndiyo?”
“Ndiyo.”
“Basi nataka mkifumba macho, kila mmoja avute picha na kuanza kujiona kama yupo pale hospitalini na mtulize akili hapohapo, tumeelewana?” alisema mama wawili, wote tukatii alichotuambia, tukaweka duara na kushikana mikono, kila mmoja akawa anavuta hewa na kuitolea mdomoni kama alivyotufundisha.
Ndani ya dakika mbili tangu tukae mkao huo, kuna mambo ya ajabu yalianza kunitokea, mapigo ya moyo yakawa yanazidi kwenda mbio kuliko kawaida kutokana na kile nilichokuwa nakishuhudia.

MICHIRIZI YA DAMU – 16


Akapelekwa katika chumba ambacho alitakiwa kukaa kwa siku zote ambazo angesubiri safari ya kwenda nchini Marekani. Moyo wa Fareed ulikuwa na furaha tele, hakuamini kama kweli alikutana na familia ya watu waliokuwa na upendo mkubwa kama watu hao.
“Jisikie huru!” alisema mzee huyo.
“Nashukuru sana!”
Mzee Al Fakh akaondoka na kwenda chumbani kwake, alipofika, haraka sana akachukua simu yake na kupiga namba fulani. Baada ya kupokelewa tu akaanza kuongea na mtu aliyekuwa upande wa pili.
“Nimefanikiwa kumpata mmoja, anaonekana kuwa na hamu ya kufika nchini Marekani! Ndiyo! Sasa huyo ndiye tutakayembebesha mabomu kwenda kulipua jijini New York katika kituo cha treni cha Pennsylvania. Haina shida, ataingia kama kawaida na hakuna ambaye atamshtukia, wasiliana na Hassan Bin Latif umpe maelekezo ya kumpokea mtu huyu na kumuelekeza ni kitu gani anatakiwa kufanya. Inshallah!” alisema Mzee Al Fakh na kukata simu.
****
Zaidi ya watu hamsini walifariki dunia katika mgahawa mmoja huko Amsterdam nchini Uholanzi baada ya bomu kulipua eneo hilo lililokuwa limekusanya watu wengi. Hiyo ilikuwa taarifa iliyoishtua dunia, ilikuwa ni idadi kubwa ya watu kuliko milipuko yote ambayo iliwahi kutokea katika nchi za Ulaya.
Watu walikuwa wakiendelea kujitoa mhanga, lilikuwa tukio baya la kujitoa mhanga ambalo lilitokea mwaka huo. Watu walilalamika, kundi la kigaidi la Al Qaeda lilijitokeza hadharani na kutangaza kwamba wao ndiyo walikuwa wamehusika katika mlipuko huo.
Marekani ikachukia, kila siku ilijitahidi kupambana na ugaidi, magaidi walikamatwa na kupelekwa katika gereza lililojaa mateso la Guantanamo lakini ugaidi haukupungua. Watu wengi, hasa vijana wa Kiarabu walikuwa wakikamatwa, walifundishwa kufanya matukio ya kigaidi huku akili zao zikijengwa kisaikolojia kwamba kuua katika ugaidi hakukuwa dhambi bali ni kuitetea dini.
Vijana wengi wa Kiarabu wakaingia katika mkumbo huo, waliahidiwa mambo mengi kwamba familia zao zisingepata shida tena na kama wangejitoa mhanga siku hiyohiyo wangekuwa peponi, pembeni ya mtume wakifarijiwa kwa kazi kubwa waliyoifanya duniani.
Hiyo ndiyo ilikuwa mbinu nyepesi ya kuwapata vijana wengi na wakafanikiwa hivyo kujitoa mhanga. Dunia ilionekana kubadilika, amani ikapotea, nchi nyingi za Ulaya zikawa na hofu na watu kutoka Mashariki ya Kati kwamba hawakuwa watu wa kuaminika na muda wowote ule wangeweza kufanya mauaji.
Kwa kipindi kirefu kundi hilo la kigaidi likatamani kulipua Marekani. Walikumbuka jinsi walivyotumia ndege mwaka 2001, hawakutaka kuridhika hivyo kutamani kulipua tena kwani waliamini kwamba wanaonewa, walitaka kuyaondoa majeshi ya Marekani na Uingereza nchi mwao, kitu pekee kuonyesha kwamba walichukizwa na uwepo wao huko kilikuwa ni kuwalipua tu.
Hawakujua ni kwa jinsi gani wangeweza kuingia nchini Marekani. Waliwatumia watu wengi kwenda huko lakini ilishindikana, hata kabla hawajaingia nchini Marekani, walikamatwa na hivyo kufungwa katika gereza la Guantanamo. Walijiuliza ni sababu zipi ziliwafanya kukamatwa kirahisi namna hiyo na jibu pekee walilolipata ni kwa sababu waliwatumia Waarabu wenzao.
Ili kuingiza bomu nchini Marekani ilitakiwa kumtumia Mzungu au mtu mweusi, hawakujua wangewapata vipi, kwa Wazungu ilikuwa vigumu sana lakini kwa watu weusi halikuonekana kuwa jambo gumu hata kidogo.
Wakakutana nchini Uturuki, nchi pekee barani Ulaya ambayo walikuwa wakikaa kwa usalama kwa kuwa watu wa nchi hiyo walikuwa Waarabu wenzao. Hapo ndipo walipopanga mipango, wakawafuata watu weusi waliotaka kuingia Marekani, waliwaambia kwamba walikuwa tayari kuwasaidia lakini walipowaambia kuhusu mabomu, waliogopa.
Walipoteza watu wengi, wakaweka vikao na kuona kwamba hawakutaka kuwaambia lengo la kuingia nchini Marekani bali walitakiwa kubaki kimya, wawape mizgo ya mabomu pasipo wao wenyewe kujua.
Kitendo cha Fareed kupatikana kiliwapa uhakika kwamba mwanaume huyo angefanikiwa kuingiza mabomu nchini humo, mawasiliano yakafanyika na hivyo taarifa kupelekwa kwamba tayari kijana mmoja alikuwa amepatikana, kijana aliyekuwa na hamu ya kuingia nchini Marekani.
“Hata mimi ninao wawili huku,” alisikika kijana aliyeitwa Mohammed Mustapha, mwanaume aliyekuwa akipanga safari za kwenda nchi mbalimbali kulipua.
“Safi sana. Basi nitaomba uje kumchukua na huyu,” alisema Mzee Al Fakh.
“Haina shida.”
Fareed hakuwa na hofu, moyo wake ulifurahi mno kwa kuona kwamba hiyo ndiyo ilikuwa nafasi yake ya kuelekea nchini Marekani. Hakuhisi kama watu hao walikuwa wabaya waliotaka kumbebesha mabomu mpaka nchini MArekani.
Mzee Al Fakh alipokuwa akizungumza naye, aliongea kiupole mno kiasi kwamba wakati mwingine Fareed alihisi kwamba mzee huyo alikuwa malaika aliyejivisha mwili wa binadamu.
Akalala na siku iliyofuatia, Mustapha akafika nyumbani hapo ambapo akatambulishwa kwa Fareed na hivyo kumchukua tayari kwa kuondoka naye kuelekea sehemu na kupanga safari hiyo.
Nyumbani kwa Mustapha akakutana na wanaume wengine wawili ambao hao nao walitakiwa kuondoka nao kuelekea nchini Marekani, vijana hao walikuwa weusi kama yeye, walikuwa wametoka nchini Senegal na wao walitamani kuingia nchini Marekani na kufanya mambo yao.
Siku hiyo wakasalimiana, wakazoeana na kulala pamoja. Usiku walizungumza mambo mengi, kila mmoja alimwambia mwenzake jinsi alivyosumbuka mpaka kufika nchini Uturuki. Kila mmoja alipitia msoto mkali mpaka kufika hapo. Kila walipoongea, waliwashukuru Waarabu hao, walionekana kuwa watu wazuri waliokuwa na lengo la kuwasaidia kufika nchini humo.
Walikaa pamoja kwa siku mbili tu kisha wakachukuliwa na kupelekwa sehemu iliyokuwa na makontena mengi. Wakaambia kwa sababu walitaka kuzamia nchini humo ilikuwa ni lazima waingie kupitia makontena hayo ambayo kwa ndani kulikuwa na kiyoyozi ambacho kingewafanya kuwa salama kipindi chote hicho.
Humo ndani, waliwekewa mabegi madogo ya mgongoni ambayo yalikuwa na vitu ndani, hawakujua kulikuwa na nini ila waliambiwa kwamba ile ilikuwa ni mizigo ambayo walitakiwa kuipeleka sehemu fulani ambapo huko wangekutana na mtu ambaye angewaambia ni nini cha kufanya.
Kwa New York ambapo walitakiwa kwenda, waliambiwa kabisa kwamba safari yao ingekwenda mpaka katika kituo cha treni cha Pennsylvania kilichokuwa jijini New York, watakapofika hapo, kuna mtu angewafuata na kuzungumza nao kisha kuondoka zake.
Hilo halikuwa tatizo, walichokuwa wakikihitaji ni kufika nchini Marekani tu. Hawakupoteza muda safari ikaanza kuondoka hapo Uturuki kwenda nchini Marekani. Kwa usafiri wa meli hiyo, wangetumia mwezi mmoja njiani mpaka kufika huko.
“Mwezi mmoja?” aliuliza Fareed.
“Ndiyo!” alijibu Mustapha.
“Ni kipindi kirefu mno, kweli hatuwezi kutumia hata wiki moja au chini ya hapo?” aliuliza Fareed.
“Ila ni mbali sana.”
“Ndiyo! Ila mwezi mzima nao ni mwingi mno,” alisema Fareed.
Hawakuwa na jinsi, hakukuwa na uwezekano wa kuwahi huko, ilikuwa ni lazima watumie mwezi mzima mpaka kufika nchini humo. Hawakuwa na hofu, walichojua ni kwamba walikuwa katika mikono salama na kusingekuwa na tatizo lolote lile.
Hawakutaka kujiuliza sana kuhusu mabegi madogo ambayo waliambiwa kwamba ni lazima waingie nayo nchini Marekani na kukutana na mtu ambaye aliwaambia kwamba wangekutana naye. Walimwamini Mustapha, kila mtu ambaye walikutanishwa naye, walimwamini kwa asilimia mia moja.
Safari ikaanza, ilikuwa ni ndefu na yenye kuchosha mno lakini hawakujali. Wiki ya kwanza ikakatika wakiwa majini, ya pili, ya tatu mpaka ya nne bado walikuwa njiani kuelekea nchini Marekani kwa kupitia katika Bahari ya Atlantiki.
Baada ya kupita siku ishirini na nane, wakaingia katika Visiwa vya Puerto Rico ambapo walipokelewa kinyemela na Waarabu wengine na kupelekwa katika nyumba moja kubwa na kutulia huko.
Bado waliendelea kuwaona Waarabu kuwa watu wema, hawakujua mpango mzito waliokuwa nao watu hao, hawakujua kama walikuwa wakienda kutolewa mhanga pasipo wao kujua.
Hapo Puerto Rico walikaa kwa siku mbili kisha kuondoka na kuelekea nchin Cuba ambapo hapo wakakutana na Waarabu wengine waliowaunganisha kwa baadhi ya wanajeshi na kuambiwa lengo la watu hao kufika hapo.
Kutokana na uadui mkubwa baina ya Marekani na Cuba, mipango ikaanza kusukwa upya, ilikuwa ni lazima Marekani ilipuliwe kwa mara nyingine tena na watu hao ndiyo waliowafanyia mpango Fareed na wenzake kuingia nchini Marekani kinyemela kabisa, njia walizokuwa wakitumia Wacuba hasa wauza unga na kutulia jijini New York.
“Kesho mtaelekea katika Kituo cha Pennslyvania, hapo kuna treni itakuja, kuna mtu atawaletea tiketi na nyie kuondoka, popote mtakapokwenda mtajua kivyenuvyenu, cha msingi tumekwishawaleta Marekani, sasa kutafuta maisha ni juu yenu,” alisema Mustapha huku akiwaangalia.
“Tunashukuru sana!” waliitikia huku wakiwa na furaha.
“Kesho ndiyo mtakwenda. Jiandaeni!”
“Sawa.”
****
Mustapha aliwapanga vijana wake ambao walitakiwa kuwapokea wakina Fareed ambao ndiyo wangekwenda katika kituo cha treni cha Pennslyvania kwa ajili ya kulipua kituo hicho.
Siku ambayo ndiyo ingekuwa siku ya tukio, vijana wa Mustapha ambao ndiyo wangeyaseti mabomu hayo tayari walifika katika kituo hicho kwa ajili ya kuwasubiri vijana waliokuwa na mabomu kwa ajili ya kuyalipua pasipo wao wenyewe kugundua kitu chochote kile.
Wakati hayo yote yakiendelea, Fareed alikuwa katika chumba kimoja na vijana wenzake, walikuwa wamejiandaa kwa ajili ya kwenda kulipua kituo hicho cha treni pasipo kujua kama ndani ya mabegi hayo kuliwa na mabomu.
Baada ya kupewa kiasi fulani kama kuwalaghai kwamba sasa wangekwenda huko na kuanza maisha yao, wakaelekea nje ambapo wakapanda gari na Mustapha na kwenda katika kituo hicho. Hakukuwa mbali sana, hawakutumia muda mrefu wakafika ambapo moja kwa moja wakaingia ndani.
Hakukuwa na mtu aliyejua kitu chochote kile, kila aliyekuwa akiwaangalia, alijua kwamba watu hao walikuwa abiria kama wengine. Walijichanganya na watu wengine na wao kusubiri treni ambayo ingefika mahali hapo muda si mrefu.
Bango kubwa lililokuwa mahali hapo lilikuwa likionyesha dakika zilizokuwa zimebaki kabla ya treni hiyo kufika katika kituo hicho. Watu walijikusanya, bango hilo lilionyesha kwamba ziliokuwa zimebaki dakika tano tu kabla ya treni hiyo kuchukua abiria kwenye kituo hicho na kuondoka.
Kila mmoja macho yake yalikuwa yakiangalia saa yake, kwa Fareed, alikosa amani, wenzake walikuwa wakifurahi kwamba hatimaye maisha yao yangeanza nchini Marekani lakini kwake, kila dakika zilipokuwa zikienda mbele ndivyo alivyokuwa na hofu zaidi.
“Humu ndani ya mabegi kuna nini? Kwa nini hawakuturuhusu tufungue ili tuangalie? Kama kuna kitu kizuri, hivi kweli wasingependa tujue?” alijiuliza Fareed huku akijaribu kujiuliza juu ya kile kilichokuwa ndani ya begi.
Muda huo Mustapha alikuwa pembeni yao, macho yake yalikuwa katika saa aliyokuwa ameivaa. Huku zikiwa zimebaki dakika tatu hata kabla ya treni kufika, Mwarabu mmoja akafika mahali hapo na kusimama pembeni ya Mustapha na kuanza kuzungumza naye.
Fareed alisikika lakini hakufahamu watu hao walikuwa wakizungumzia mambo gani. Mwanaume huyo aliyekuwa akizungumza na Fareed alikuwa na kifaa kama rimoti mkononi mwake, hakujua kazi ya hicho ila kwa jinsi kilivyoonekana, alijua kwamba hakikuwa kitu kizuri.
“Guys! I think this is our last time to meet each other! Have the good journey,” (jamani! Nafikiri huu ndiyo mara ya mwisho kuonana sisi nanyi! Muwe na safari njema) alisema Mustapha huku akiwaangalia wanaume hao.
“Thank you sir,” (ahsante bwana mkubwa)
Mustapha na yule mwanaume hawakutaka kusubiri mahali hapo, wakaondoka mahali hapo na kuelekea nje ya kituo hicho. Fareed na wenzake wakabaki kituoni hapo wakiwa na mabegi yale yaliyokuwa na mabomu.
Bado kichwa chake kilikuwa na mawazo tele, alikuwa na maswali mfululizo juu ya kile kilichokuwa ndani ya mabegi yale. Hakutaka kuridhika, akawaaga wenzake kwamba anakwenda chooni kujisaidia na angarudi muda si mrefu.
Akaondoka harakaharaka, alipofika chooni, kitu cha kwanza kilikuwa ni kuliweka chini lile begi, zipu zilifungwa kwa kufuli ndogo alichokifanya ni kulichana, ndani, akakutana na mfuko mweusi na alipoufungua, macho yake yakatua katika bomu moja kubwa lililokuwa likiwaka kitaa chekundu.
“Mungu wangu!” alisema kwa mshtuko, ghafla akasikia huko nje treni ikiwa inaingia, muda ambao bomu hilo lilitakiwa kulipuliwa.
****
Mustapha na mwenzake wakatoka nje, wakaelekea kwenye gari lao huku akiwa na furaha tele. Moyo wake aliona kwamba alifanikiwa katika kile walichokuwa wamekipanga kwamba mabomu yalifika salama nchini Marekani na muda huo yalikuwa kituoni.
Wakalifuata gari lao na kutulia humo. Mudda wote macho yao yalikuwa katika saa zao huku masikio yao yakisikiliza kwa makini kile kilichokuwa kikiendelea katika kituo kile. Kama treni ingekuwa inaingia kituoni hapo, kusingekuwa na ugumu wa kujua hilo, wangesikia mlio wake na hivyo kukaa kwa sekunde chache, litakaposimama tu waweze kulipua bomu hilo.
“Muda unakwenda tu! Subiri tusubiri,” alisema Mustapha.
Walisubiri kwa dakika tatu tu wakasikia treni likiwa linaingia, hawakutaka kuwa na presha kubwa, walisubiri mpaka waliposikia limesimama na abiria kuanza kuteremka. Mwanaume aliyekuwa na Mustapha akachukua kirimoti kile kwa lengo la kulipua mabomu yale.
“في سبيل الله,” (kwa ajili ya Mungu) alisema mwanaume yule kisha kubonyeza kitufe kile.
“Puuuuuuuu…..” ilisikika milio ya mabomu makubwa matatu yaliyopuka ndani ya kituo hicho.
****
Bilionea Belleck alikuwa na kila kitu, kila siku alikuwa akikusanya fedha nyingi kutokana na biashara mbalimbali alizokuwa akizifanya. Aliingiza kiasi kikubwa cha fedha na kila siku katika maisha yake aliendelea kuogelea kwenye dimbi kubwa la utajiri.
Alipendwa kutokana na sura nzuri aliyokuwa nayo, alipendwa kutokana na utajiri mkubwa aliokuwa nao. Kila siku kazi yake ilikuwa ni kubadilisha wanawake, alikuwa akienda kununua wanawake barabarani na kwenda kufanya nao mapenzi.
Aliyazoea maisha hayo, hakutaka kutulia nyumbani, alikuwa mtu wa safari, kusafiri kuelekea Ufaransa, Uholanzi, Italia, kila alipokuwa ilikuwa ni lazima kulala na wanawake kitu ambacho alipenda kufanya katika maisha yake.
Hakumfikiria mtu aliyeitwa Fareed, kwake, alijua kabisa mtu huyo hakuwepo katika uso wa dunia, alikumbuka jinsi alivyowatuma watu na kwenda kumtupa baharini, tena hakutupwa huku wakiwa watu hao, alitupwa huku akishuhudia kitu kilichompa uhakika kwamba mtu huyo alikuwa chakula cha samaki mpaka muda huo.
Baada ya kupata sana pesa, hatimaye yeye kama bilionea alitakiwa kukutana na mabiliona wenzake nchini Ufaransa kwa ajili ya kujadili biashara zao, huo ulikuwa mkutano mkubwa ambao kwa bilionea kama yeye ilikuwa ni lazima kushiriki na kuangalia ni kwa namna gani wangeweza kufanikiwa zaidi katika biashara zao na kuweka ubia na mabilionea wa Kiarabu kwa ajili ya kupanua soko lao.
Kikao kikafanyika nchini humo, kilikuwa kizito, kikubwa ambacho kilitangazwa na vyombo mbalimbali vya habari. Kikao hicho kilitakiwa kuchukua wiki moja kwani kulikuwa na mada nyingi, na kwenye kila mada ilikuwa ni kuwapendelea wao na si watu masikini ambao waliwafanya kuwa hapo.
Kwa sababu machangudoa walijua kwamba mabilionea walikuwa wateja wao wakubwa, wakawa wanakusanyika nje ya Hoteli ya King Napoleon II kwa ajili ya kuwanunua na kwenda kulala nao.
Kama ilivyokuwa kwa mabilionea wengi, kila siku ilikuwa ni lazima kwa Bilionea Belleck kuchukua changudoa na kuondoka naye kulala naye usiku mzima. Alikuwa na pesa, alikuwa na kila kitu alichokuwa akikihitaji katika maisha yake, hakuona kama kulikuwa na ugumu wa kulala na mwanamke yeyote aliyekuwa akimuhitaji katika kipindi hicho.
“Unaitwa nani?” aliuliza mara baada ya kumfuata msichana mmoja kisri.
“Natalie!”
“Ooh! Gharama zako zipo vipi?”
“Euro elfu moja!”
“Sawa!”
Hakuwa na mazungumzo marefu, alijiamini, hakuona kama kulikuwa na changudoa ambaye angemtajia gharama ya pesa ambazo hakuwa nazo. Akamchukua msichana huyo na kuondoka zake.
Hakutaka kuwa na wapambe, alitaka kufanya kila kitu peke yake, aliamini kwamba kama angekuwa na wapambe mambo yangevuja na hatimaye kujulikana kama alikuwa akinunua machangudoa kitu ambacho hakutaka kabisa kijulikane kwa kuogopa kumuumiza mkewe.
Machangudoa wengi walipenda kununuliwa na mzee huyo kwa sababu alikuwa na uhuru wa kukwambia wewe mwenyewe upange bei. Walipokuwa wakiliona gari lake, walilikimbilia na kujipanga mstari na hivyo kuchagua ni yupi alitakiwa kulala naye usiku wa siku hiyo.
Baada ya wiki moja kumalizika na mkutano huo kuisha, hakutaka kuondoka nchini Ufaransa, alitaka kuendelea kubaki mahali hapo kwani kulimteka, wanawake wazuri waliokuwa katika Jiji la Paris walimdatisha kichwa chake na hivyo kutamani kuendelea kukaa zaidi.
****
Kila kitu alichokuwa akikifanya ndani ya choo kile, Fareed alikifanya harakaharaka, hakutaka kuchelewa kwani kwa jinsi bomu lile lilivyoonekana, halikuwa limebakiza dakika nyingi kulipuka.
Akaliacha begi palepale chini na kisha kukimbia kutoka chooni hapo, hakutaka kubaki ndani ya kituo hicho kwani aliamini kwamba endapo angebaki basi naye pia angeweza kufa.
Kila mtu alibaki akimshangaa, wengine walihisi kwamba alikuwa mwizi, kwamba aliiba na hivyo kukimbia. Sehemu ambayo ilikuwa ikijifungua kwa kichuma kwenda juu baada ya kuweka tiketi, hakutaka hata ijifungue, akaruka kwa juu na kuelekea nje.
Wakati anafika nje ya kituo hicho kwa kupitia mlango mwingine, mabomu yakasikika yakilipuka na nguvu yake ilikuwa kubwa kiasi kwamba mpaka wao waliokuwa nje ya kituo kile wakarushwa akiwepo yeye mwenyewe.
Akaangukia katika gari moja lililokuwa limepaki pembeni, watu wengine waliokuwa hapo walikuwa hoi, wengine walikuwa wakiteketa kwa moto, pale alipoangukia ambapo kulikuwa ni kama hatua kumi kutoka pale alipokuwa amefikia, Fareed alikuwa hoi, kichwa chake kilikuwa kikitoka damu, alisikia maumivu makubwa mwilini mwake.
Akajitahidi kusimama, akashindwa, akabaki hapohapo akiwa amelala huku macho yake yakiwa mazito kabisa. Akajitahidi kuuinua mkono wake, akashindwa, kila kitu alichotaka kukifanya mahali hapo alishindwa kabisa.
Kwa kutumia uangaliaji wake wa kwa mbali, akawaona watu wakikimbia huku wakipiga kelele za kuomba msaada, baada ya sekunde ishirini tu akiwa hapo, giza kubwa likayafumba macho yake na baada ya sekunde hizo, akapoteza fahamu na hakujua kitu gani kiliendelea.
****
Lilikuwa tukio kubwa lililoishtua dunia, hakukuwa na mtu aliyeamini kama kweli Marekani ingeweza kulipuliwa kama ilivyotokea. Kila mtu alishangaa kwani kwa jinsi nchi hiyo ilivyokuwa imejiwekea ulinzi tangu kulipuliwa kwa maghorofa ya biashara ya WTC, hakukuwa na aliyeamini kwamba kweli magaidi wangeweza kuilipua nchi hiyo kwa mara nyingine.
Watu zaidi ya elfu moja mia tano wakasadikiwa kufa  katika tuki hilo huku maelfu wakijeruhiwa vibaya. Ndani ya dakika chache tangu tukio hilo litokee, magari ya zimamoto yakafika mahali hapo yakiongozana na magari kadhaa ya wagonjwa.
Polisi wakaweka kamba ya nyano iliyoandikwa ‘Do not cross’ yaani Usivuke huku ni polisi tu na watu wa afya ndiyo walioruhusiwa kwenda ndani ya kituo kile kulipotapakaa miili mingi ya watu.
Mambo yote hayo yalikuwa yakiendelea huku Fareed akiwa chini, hakujitambua, pale alipokuwa, kwa jinsi alivyokuwa amerushwa, ilikuwa vigumu kuamini kama mtu huyo alikuwa mzima.
Yeye na majeruhi wengine wakachukuliwa na kukimbizwa hospitali kwa ajili ya matibabu huku nyuma waandishi wa habri wakiendelea kukusanyika katika eneo hilo la tukio kwa ajili ya kuripoti kila kitu kilichokuwa kikiendelea.
Gari halikuchukua muda mrefu likafika katika Hospitali ya St. Joseph Medical Centre iliyokuwa hapohapo Pennsylvania ambapo mara baada ya magari kuingizwa ndani, machela zikaletwa, majeruhi wakapandishwa kwenye machela hizo kisha kupelekwa ndani.
Hiyo ndiyo ilikuwa siku ya kwanza kwa Fareed kukaa ndani ya hospitali hiyo. Matibabu yalikuwa yakiendelea kama kawaida. Baada ya saa kumi na mbili, akarudiwa na fahamu, akayafumbua macho yake na kuanza kuangalia huku na kule.
Mahali pale palikuwa ni hospitali, hakujua alikuwa amefikaje, aliangalia huku na kule, kwa juu, dripu ilikuwa ikining’inia huku mwili wake ukiwa na maumivu makali kiasi kwamba alishindwa hata kugeuka.
Mbali na yeye, ndani ya wodi ile kulikuwa na wagonjwa wengine ambao hawakuonekana kuwa na nafuu kama alivyokuwa. Huo haukuwa mwisho wa safari yake, ilikuwa ni lazima aondoke mahali hapo, alitaka kwenda sehemu kwa ajili ya kukaa kisha kumtafuta Bilionea Belleck ambaye aliamini kwamba bado alikuwa hapohapo Marekani.
“Ni lazima niondoke hapa,” alisema Fareed.
Kuondoka mahali hapo haikuwa kazi nyepesi, mara kwa mara madaktari na manesi walikuwa wakifika kwa ajili ya kuangalia maendeleo yao. Hakutaka kabisa kuendelea kubaki kwani bado maisha yake aliyaona kuwa na hatari kubwa.
Kwa kuwa kulikuwa na ugumu wa kufanya hivyo, kitu chepesi alichokifanya ni kusubiri mpaka usiku ambapo akaomba nafasi ya kwenda chooni kwa lengo la kufika huko na kukimbia zake.
Akasimama na kutembea kwa mwendo wa taratibu, mwendo ulioonyesha kwamba hakuwa mzima kiafya, alipofika chooni, akajisaidia haja ndogo na kuangalia ni kwa namna gani angeweza kutoroka hospitali hapo pasipo kuonekana.
**
Bado watu waliendelea kushangaa juu ya tukio la kigaidi lililokuwa limetokea nchini Marekani. Shirika la kipelelezi la FBI lilikuwa kwenye wakati mgumu, hawakujua ni kwa jinsi gani wangeweza kuwapata wahusika wakuu wa tukio hilo ingawa Al Qaida walijitokeza hadharani na kusema kwamba wao walihusika kwa kila kitu.
Walichokuwa wakikihitaji FBI ni picha zilizokuwa zimepigwa dakika kadhaa kabla ya tukio kutokea. Ilikuwa ni lazima waangalie kwenye kamera za CCTV kuona kila kitu kilichokuwa kimetokea humo.
Wakaelekea katika chumba kilichokuwa na kompyuta nyingi, zilikuwa zimeunguzwa vibaya lakini walichoshukuru Mungu ni kwamba memory cards zote ambazo zilikuwa zimechukua picha kutoka ndani ya kituo hicho kabla ya tukio la kmlipuko kutokea, zilikuwa salama kabisa.
Wakazichukua na kuelekea katika kompyuta zao na kuangalia kuona kama wangeweza kuwaona wahusika wa mlipuko ule. Walifanikiwa kumuona Fareed na wenzake, waliwahisi kwamba hawakuwa na nia nzuri kutokana na mabegi ya kufanana waliyokuwa nayo. Baada ya dakika kadhaa, wakamuona Fareed akiondoka.
“Let’s roll with him,” (twende naye huyo) alisema Frankline, mmoja wa FBI waliokuwa wakifuatilia tukio hilo.
Kwa kutumia kamera mbalimbali waliweza kumfuatilia Fareed aliyekuwa akikimbia, alipofika chooni, akaingia na kisha kutoka na kuendelea kukimbia. Wakahisi kwamba huyo ndiye aliyekuwa amehusika na mlipuko ule, wakaendelea kumfuatilia mpaka nje, kituo kikalipuka, na yeye mwenyewe akarushwa na kujipigiza katika gari moja.
“Take his picture,” (chukua picha yake) alisema Frankline na mwenzake kufanya hivyo, walivyoikuza, wakamgundua, picha ikaprintiwa na mpaka gari la wagonjwa lilipomchukua na kuondoka naye, walikuwa wakifuatilia kila kitu.
“Which hospital?” (hospitali gani?)
“St. Joseph!”
“Let’s go…let’s go,” (twendeni…twendeni) alisema Franckiline, maofisa wanne wa FBI waliokuwa na bunduki wakaanza kwenda kwenye hospitali hiyo kwa ajili ya kumkamata Fareed ambaye walikuwa na uhakika kwamba alihusika kwa asilimia mia moja katika mlipuko huo.
Wakawapa wenzao taarifa juu ya kile kilichokuwa kimetokea, hawakuishia kuwataarifu bali wakawatumia na picha za mwanaume huyo na kwamba walikuwa njiani kwenda kumkamata.
Kwa kuwa mahali hapo hakukuwa mbali na hospitali, ndani ya dakika kumi wakafika na moja kwa moja kuingia ndani. Kulikuwa na idadi kubwa ya watu, wengi waliokuwa mahali hapo walifika kwa ajili ya kuwaona ndegu zao waliokuwa hoi.
Wakazungumza na madaktari na kumuonyeshea picha ya Fareed, kwa kuwa daktari huyo alikuwa akiwakumbuka watu aliokuwa amewapokea, hakukuwa na ugumu kugundua kwamba picha ya mtu aliyekuwa ameonyeshewa alikufikishwa ndani ya hospitali hiyo saa moja iliyopita.
“Where is him?” (yupo wapi?)
“Come with me,” (nifuateni) alisema daktari huyo na kuanza kumfuata.
Daktari yule akawapeleka mpaka katika wodi aliyolazwa Fareed ambapo akawakabidhi watu hao kwa nesi aliyekuwa akiwahudumia wagonjwa waliokuwa katika wodi hiyo. Alipoonyeshewa picha ya Fareed, alimgundua kwani alikuwa miongoni mwa wagonjwa waliokuwepo humo ndani.
“I know him,” (namfahamu)
“Where is he? (yupo wapi?)
Nesi yule akawachukua mpaka katika kitanda alicholazwa Fareed, walipofika, mwanaume huyo hakuwepo na alipomuuliza nesi mwenzake akamwambia kwamba Fareed alikuwa amekwenda chooni.
“Where is the toilet?” (choo kipo wapi?)
“Come with me,” (nifuateni) alisema na kuanza kumfuata nesi huyo kwenda huko chooni.
****
Maofisa wale wa FBI na nesi yule wakafika ndani ya choo kile, wakaangalia huku na kule, mtu waliyekuwa wakimtafuta hakuwepo humo. Nesi alishindwa kuelewa kwamba ilikuwaje Fareed asiwe humo na wakati alimuona akielekea chooni na hakuwa na uhakika kama mwanaume huyo alikuwa ametoka.
FBI hawakutaka kuridhika, walijua kwamba mwanaume huyo alikuwa ndani ya vyoo hivyo, wakaendelea kumtafuta kwenye kila choo lakini hawakuweza kumuona.
Hawakutaka kukata tamaa, waliamini kwamba kama mwanaume huyo hakuwa chooni humo basi atakuwa ametoka, na kama ni kipindi kifupi kilichopita waliamini kwamba hakuwa mbali kutoka mahali hapo.
Wakaelekea sehemu zingine ndani ya hospitali hiyo lakini hawakuweza kumuona Fareed, wakaelekea mpaka nje kabisa lakini kila kona waliyoangalia, mwanaume huyo hakuonekana machoni mwao.
“Where is he?” (yupo wapi?) aliuliza ofisa mmoja.
“I don’t know! He just went to the toilet,” (sijui! Alikwenda chooni) alijibu nesi.
****
Fareed alikuwa chooni, moyo wake haukuwa na amani hata kidogo, aliamini kwamba ilikuwa ni lazima kutafutwa kwani alikumbuka kwamba katika kituo kile cha treni kulikuwa na kamera ndogo za CCTV hivyo kugundulika lilikuwa suala jepesi sana.
Hakutaka kubaki humo, ilikuwa ni lazima kuondoka kuelekea popote pale lakini si kuona akikamatwa kwa kufanya jambo ambalo alilazimishwa kulifanya pasipo kujua kama lilikuwa kosa lolote lile.
Akaondoka na kuelekea nje ya choo kile, hakutaka kuonekana, aliondoka mpaka kufika nje huku akikutana na madaktari wengi ambao hawakumuuliza kitu chochote zaidi ya kumuacha tu.
Alijipekua mfukoni, alikuwa na kadi yake ya benki ambayo ilimuwezesha kuchukua kiasi chochote cha pesa sehemu yoyote ile. Akaelekea mpaka katikakibanda cha ATM na kutoa kiasi cha dola mia tano na kuondoka zake.
Safari yake iliishia katika hoteli ya kawaida ya Windows iliyokuwa hapohapo Pennyslvania, akachukua chumba ambacho alitakiwa kulipa dola mia mbili hamsini, zaidi ya laki tano kwa usiku mmoja tu.
Hilo halikuwa na tatizo, alikuwa na kiasi kikubwa cha fedha ambacho angeweza kufanya jambo lolote lile, hivyo akaelekea katika chumba hicho. Hakulala, alibaki akifikiria namna alivyonusurika kuuawa kwa kulipukiwa na bomu.
Moyo wake ukawa na ghadhabu, akawa na hasira na Waarabu kwani aliamini kwamba watu hao hawakuangalia utu, hawakujua ni watu wangapi waliwakosea, katika kuua, waliua kila mtu hata kama hawakuwa na hatia kama alivyokuwa.
Hakutaka kuwafikiria sana Waarabu, alichokitaka ni kusonga mbele na kutekeleza kile alichokuwa akikitaka. Aliingia nchini MArekani kwa lengo la kumuua Bilionea Belleck ambaye aliamini kwamba alikuwa nchini humo.
Akaanza kufuatilia, alikuwa na marafiki wachache nchini humo ambao wangekuwa na data zote kuhusu bilionea huyo na kwa jinsi gani angeweza kumpata. Kwa kuwa bilionea Belleck alikuwa na maadui wengi akiwemo bilionea mwenzake, Peter Williams, alichokifanya ni kumpigia simu.
“Unanikumbuka?” alimuuliza bilionea huyo ambaye aliwahi kutambulishwa na Bilionea Belleck kabla ya wawili hao kutofautiana kwenye mambo ya kibiashara.
“Hapana!”
“Kwa hiyo namba yangu uliifuta?” aliuliza Fareed.
“Mmh! Sina uhakika! Wewe nani?”
“Naitwa Farida!”
“Yupi?”
“Yule wa Belleck!”
“Ooh! Yule wa mpumbavu?”
“Ndiyo!”
Kwa sababu watu hao walikuwa wakichukiana, Fareed aliamini kwamba angeweza kufanya naye kazi kwa ajili ya kukamilisha kile alichokuwa akikihitaji. Akamwambia mwanaume huyo kwamba walitakiwa kuonana na hivyo kama hatojali basi aende kuzungumza naye kitu ambacho kwa bilionea huyo hakukuwa na tatizo lolote lile.
Ndani ya saa moja tayari Bilionea William alikuwa mbele ya Fareed. Alimwangalia kwa umakini sana, alionekana kuwa mtu tofauti kabisa, hakuwa kama kipindi kilichopita, mwanaume mwenye muonekano wa kike, kwa kipindi hicho alikuwa mwanaume shupavu, mwenye mwili uliojazia.
Williams alibaki akimkodolea macho, hakuamini kama mwanaume aliyesimama mbele yake ndiye mwanaume yule aliyefahamiana naye kitambo. Fareed akamwambia bilionea huyo kile kilichomleta Marekani, hakuja kula starehe bali alitaka kufanya kazi moja, kumuua Bilionea Belleck.
“Kwa nini tena?”
Akamwambia sababu kwamba aliamua kufanya hivyo kwa kuwa mwanaume huyo naye alitaka kumuua ila kwa msaada wa Mungu aliweza kumtoroka na watu wake.
Williams akafurahia, chuki aliyokuwa nayo kwa Belleck ilikuwa kubwa kiasi kwamba kwa kitendo cha kuambiwa kwamba mwanaume huyo alikuwa tayari kumuua halikuwa tatizo kabisa.
“Kwanza hayupo Marekani,” alisema William.
“Yupo wapi?”
“Paris nchini Ufaransa,” alijibu Williams.
“Ni lazima niende huko. Utanisaidiaje kufika?” aliuliza Fareed.
Ili apate msaada wa kufika Ufaransa ilikuwa ni lazima amwambie Williams ukweli kwamba alikuwa akitafutwa kila kona. Mwanaume huyo alibaki kimya, alitaka muda wa kujifikiria ni kwa jinsi gani angemtorosha Fareed kuelekea nchini Ufaransa.
Alikaa na kuwaza sana, jibu alilokuja nalo ilikuwa ni lazima kwa mwanaume huyo asafiri kwa kutumia ndege yake binafsi ambayo ingempeleka mpaka huko.
“You will take my flight,” (utachukua ndege yangu) alisema Williams.
Hakuwa na uamuzi mwingine zaidi ya huo na safari ilitakiwa kufanyika usiku. Fareed akajiandaa na baada ya siku mbili, magari mawili ya kifahari yakafika hotelini hapo na kumchukua kisha kumpeleka uwanja wa ndege.
Moyo wake ulikuwa na hofu, hakuamini kama angefika salama huko kwani kila kona alikuwa akitafutwa na FBI ambao hawakutaka kuzisambaza picha zake, walimtafuta kimyakimya ili asishtukie kama anatafutwa kumbe mwenzao alikwishajua hilo kitambo.
Uwanja wa ndege, hakupitishwa mlango wa kawaida, ndege ilikuwa ni ya binafsi tena ya bilionea mkubwa duniani, hivyo hata mlango aliopitishwa ulikuwa ni wa VIP na ilikuwa vigumu kumgundua kwamba alikuwa yeye.
Mpaka anakaa katika kiti ndani ya ndege hiyo, akashusha pumzi ndefu, hakutegemea kama ingekuwa kazi nyepesi namna hiyo. Huku nyuma, bilionea Williams alikuwa akifanya mawasiliano na watu wake waliokuwa Ufaransa, alitaka kupata data zote kuhusu bilionea huyo, kwamba alikuwa akiishi katika hoteli gani na ratiba yake ya siku ilikuwaje. Hilo halikuwa tatizo kwa vijana wake, kwa kuwa walikuwa huko na mtu huyo alikuwa maarufu, wakapata data zote na kumtumia na hivyo na yeye kumtumia Fareed ambaye baada ya kuzipokea, akamshukuru Mungu.
“Sasa kazi itafanyika,” alimwambia Williams kwenye simu.
“Ukikamilisha! Nakuahidi kukupa dola milioni kumi. Huyu mpumbavu ananinyima sana usingizi,” alisema William huku akiwa na uhakika kwamba ilikuwa ni lazima mwanaume huyo ammalize Bilionea Belleck. Ila la zaidi, alitaka kuona bilionea huyo akifa na yeye kumuua Fareed kwani kama angemuacha, siri ingeweza kuvuja. Ili siri itunzwe ilikuwa ni lazima hata naye Fareed afe.
****
Fareed hakujua mahali mwanaume huyo alipokuwa, ila aliambiwa kwamba angepewa maelezo yote kwani yale aliyopewa mara ya kwanza, yalibadilika kwani mtu huyo aliondoka Paris na hakukuwa na aliyejua kama alikwenda Monaco au Marseille.
Baada ya dakika hamsini akapigiwa simu na kuambiwa kwamba mwanaume huyo hakuwa hapo Paris bali alikuwa jijini Marseille katika Hoteli ya Melkizedeki ambapo alikuwa akilala huku kila siku akishiriki katika kikao cha matajiri.
Hilo halikuwa tatizo, haraka sana akaondoka hotelini alipokuwa, akachukua ndege na kuelekea Marseille ambapo ndipo aliambiwa mwanaume huyo alipokuwa. Njiani, alikuwa akimuomba Mungu afike salama kwani alikuwa na hasira kali, asingeweza kumuacha mwanaume huyo akaishi kwani alikuwa miongoni mwa watu waliotaka kumuua kwa nguvu zote.
Walichukua dakika arobaini na tano tu mpaka kufika jiji humo ambapo akateremka na kuchukuliwa kwa gari mpaka katika hoteli moja na kutulia huko. Ilipofika saa mbili usiku, wanaume wawili wakafika hotelini hapo na kuomba kuzungumza naye.
Hilo halikuwa tatizo, alipewa taarifa na Williams kwamba watu hao wangefika mahali hapo, na wao ndiyo ambao wangemwambia kuhusu Belleck ambaye hakujua alikuwa katika hoteli gani.
“Belleck yupo anakula raha, hivi tunavyoongea, keshokutwa anaondoka kurudi Marekani,” alisema mwanaume mmoja aliyejitambulisha kwa jina la De Leux.
“Sawa. Kingine?”
“Huwa anapenda sana kununua malaya mitaani! Tunajua sehemu ambayo hupenda kununua na pia tunajua hoteli anayokaa mpaka chumba alichokuwepo,” alisema De Leux.
“Haina shida! Ningependa nikutane naye na kufanya kazi yangu,” alisema Fareed.
Hakwenda huko kufanya jambo lolote zaidi ya kumuua bilionea huyo na kuondoka zake. Wanaume hao wawili ndiyo walikuwa wachora ramani wakubwa, walikuwa wakienda hotelini hapo, wanaonana na wahudumu wa hapo, wakatengeneza urafiki wa kizushi kwa ajili ya kuwasaidia hapo baadaye.
Hawakujua kama lengo la watu hao ni kumpata mwanaume aliyekuwa ndani ya hoteli hiyo. Wakati mwingine walikuwa wakikaa mapokezini, Belleck alipokuwa akiingia ndani ya hoteli ile na machangudoa walikuwa wakimuona hivyo kuwa kazi nyepesi kwao kufanya kile walichokuwa wakikitaka.
“Cha kwanza ni kupata kadi ya kufungua vyumba vyote,” alisema De Leux.
Hilo ndilo lililotakiwa, kwa kutumia uzoefu mkubwa wa kuzungumza waliokuwa nao, wakajenga ukaribu zaidi na mhudumu aliyeitwa kwa jina la Natalie ambaye bila tatizo lolote lile, naye akaukaribisha ukaribu huo na mwisho wa siku De Leux kumtongoza.
“Acha masihara wewe! Mzuri mimi?” aliuliza Natalie huku akitabasamu, japokuwa alipinga kwamba hakuwa mzuri lakini sifa zile zilimfurahisha.
“Wewe ni mzuri sana. Una tabasamu pana, msichana mrembo sana! Umeumbinka kama Mona Liza,” alisema De Leux huku akimwangalia Natalie kwa macho ya nipe nikupe.
Akamsifia usiku mzima, msichana huyo akachanganyikiwa, kila wakati akawa anapandisha juu mpaka katika chumba alichokuwa akilala De Leux na kuingia ndani. Hakutaka kufanya mapenzi na msichana huyo, kitu muhimu kilikuwa ni kuweka ukaribu na mwisho wa siku kuichukua kadi ambayo alikuwa akiitaka mno.
Wakati walipokwenda kuonana na Fareed, walimwambia kabisa kile kilichokuwa kimetokea kwamba kulikuwa na kadi moja muhimu ambayo ingewawezesha wao kuingia ndani ya chumba chochote kile.
Fareed akafurahi kwani urahisi huo ndiyo aliokuwa akiutaka kwa hali na mali. Siku hiyo wakaondoka na kwenda katika hoteli hiyo. Wakachukua chumba kwa ajili ya Fareed ambaye akaingia bila tatizo na uzembe mkubwa ambao waliufanya wahudumu wa hoteli hiyo ni kutokuishikilia passport yake.
Akaingia mpaka chumbani, akajipumzisha na kuambiwa kwamba mtu aliyetakiwa kumuua alikuwa njiani kufika mahali hapo hivyo alitakiwa kusubiri.
De Leux na mwenzake wakarudi mapokezi, wakatulia kochini. Ilipofika saa sita usiku, wakamuona Belleck akirudi hotelini hapo huku akiwa na mwanamke ambaye alivalia hijabu ila kwa nyuma alijazia hasa kiasi kwamba hata wao walipokuwa wakimwangalia walimtamani kupita kawaida.
“Huyo hapo! Subiri!” alisema De Leux.
Wakati mwanaume huyo akiingia ndani na mwanamke huyo, De Leux akamuita Natalie na kuanza kuongea naye. Alimwambia wazi kwamba siku hiyo alitaka kukaa naye na kuzungumza naye mambo mengi lakini iwe baada ya kufanya usafi katika vyumba mbalimbali.
“Haina shida mpenzi! Nitakuja,” alisema Natalie huku akionekana kuwa na furaha tele.
De Leux akaondoka na mwenzake mpaka chumbani kwake, wakakaa huko na kuyapanga kwamba siku hiyo ndiyo ilikuwa mwisho wa mtu huyo ambaye alikuwa adui wa bosi wao kwa kipindi kirefu.
Wakamfuata Fareed na kumwambia kilichokuwa kikiendelea kwamba ni yeye tu ndiye aliyekuwa akisubiriwa kufanya mauaji hayo.
“Haina tatizo!”
“Sawa. Ngoja nimuite huyu msichana alete kadi,” alisema De Leux na hapohapo kuchukua simu ya mezani na kupiga mapokezi ambapo alimtaka Natalie aende huko kuchukua shuka kwenda kulifua.



JAMANI ANTIII…NISHUSHE UNUNIO-11


ILIPOISHIA KWENYE RISASI JUMAMOSI:
“Unajua Mungu anatuvumilia kwa mengi sana, mama yangu vile, wewe niamini mimi,” Bigambo alikomelea maneno hayo yasiyofaa na kusikilizika kwa mtu mwenye akili timamu isipokuwa mlevi tu mwenye kuzidiwa na kimea kikali.

“Kweli eeh, unajua kila nikikuangalia nakutafakari sana na kuona kama wewe siyo binadamu wa kawaida, yaani nakuona kama kiumbe cha ajabu au mtu aliyewahi kuzaliwa, akafa na kufufuka tena, yaani unaishi kwa mara ya pili,” Vivian naye alijibu maneno ambayo waliokuwa wamekaa meza ya jirani kwakinywa maji na soda walianza kucheka kufuatia maneno ya Vivian kutoka kwa mpangilio usioeleweka.

Wakati wakiendelea kunywa, ghfla kuna mtu alisimama mbele yao na kumshika Vivian bega na kumuuliza alikuwa akifanya nini hapo na aliyekuwa amekaa naye ni nani kwake? Mkononi alikuwa na kitu kilichowashtua wote wawili.
SINDIKIZANA NAYO HAPA CHINI…
VIVIAN aliamka kabisa na kubaki ameshika kiti kwa mkono mmoja. Midomo ikimtetemeka kwa hasira isiyosimulika. Mtu aliyekuwa amesimama mbele yao alikuwa ni Jisu, yule fundi aliyemtengeneza mlango siku ya ugomvi wake na mzazi mwenzake, na mwisho wa siku wakaishia kushiriki dhambi tamu kutokana na kuzidiwa na kushawishiwa na vimea vya Reds na Nyagi.

Mkononi mwa Jisu kulikuwa na mzinga mkubwa wa nyagi, tena ikiwa haijafunguliwa lakini kwa macho ya harakaharaka ni kwamba Jisu alikuwa chakari kwa ulevi kwani hata ongea yake iliashiria jambo hilo kwa uwazi kabisa na pia hakuacha kuyumba na kujiweka sawa kila mara, alikuwa twiiiii, kama siyo bwiiiiiii achilia mbali bwaksiiiiii, maisha ya mitungi yana raha na karaha zake jamani.


SEVEN DAYS IN HELL (SIKU SABA KUZIMU)- 50



ILIPOISHIA:
“Ndiyo,” nilisema kwa kujiamini, akanitazama usoni kisha akaenda mlangoni na kufungua, akawaita Raya na Firyaal, wakaingia ndani na tukakaa tena kama tulivyokuwa tumekaa mwanzo, kazi ikaanza upya huku akinisisitiza kuwa makini na kuishinda hofu ndani ya moyo wangu, nikatingisha kichwa kama ishara ya kukubaliana naye.
SASA ENDELEA…
Kazi ilianza upya, akatusisitiza kila mmoja awe anavuta pumzi ndefu kwa kutumia tumbo na siyo kifua kama wengi tunavyopumua, pia akatutaka kuhakikisha kila mmoja akili yake aielekeza eneo la tukio.
Muda mfupi baadaye, ile hali ilianza kunitokea tena, nikawa najihisi kama naelea angani huku mwili mwingine ukiwa palepale tulipokuwa tumekaa. Hofu ilianza kunijia tena lakini nilipokumbuka maneno ya yule mwanamke, nilijitahidi kuishinda hofu.
Nikaendelea kutuliza kichwa na kufumba na kufumbua, nilijikuta nikiwa pale hospitalini nilipokuwa nimelazwa. Niliweza kuona kila kitu kilichokuwa kikiendelea, wagonjwa waliokuwa wakiingia na kutoka, manesi na madaktari waliokuwa wakikimbizana huku na kule kuelekea kwenye ukumbi wa mikutano.
Upande wa Kaskazini kulikuwa na magari matatu ya polisi yaliyokuwa yamepaki huku askari wengi wenye silaha wakirandaranda huku na kule.
“Kumetokea nini kwani leo hapa?”
“Nasikia kuna wagonjwa wametoroshwa usiku sasa ndiyo polisi wamekuja kutafuta wahusika.”
“Mh! Yaani wagonjwa kutoroshwa tu ndiyo zije difenda kibao na askari utafikiri kuna vita?”
“Nasikia huyo mgonjwa mmoja ni mtoto wa kigogo mmoja mkubwa ndiyo maana unaona hali ipo hivi,” niliwasikia watu wawili wakihojiana, wakiwa wamesimama chini ya kivuli cha mti.
Ghafla nikasikia vishindo vya mtu akitembea kwa kasi nyuma yangu, nikageuka, katika mazingira ambayo sikutegemea, nilimuona askari mmoja mwenye bunduki, akiwa ananifuata pale nilipokuwa nimesimama, nikajua ameshaniona na kunitambua, nikawa natetemeka.
Cha ajabu, ni kwamba alinipita akiwa ni kama hajaniona na kuwafuata wale watu waliokuwa wakiendelea na majadiliano pale chini ya mti, nikamsikia akiwapa amri kwamba hatakiwi mtu yeyote asiyekuwa na shughuli maalum kuonekana ndani ya hospitali hiyo, akawataka watoke nje ya geti na kwenda nje kabisa.
Kidogo nilishusha pumzi kwani nilikumbuka mara nyingi ninapokuwa kwenye hali kama ile, huwa siwezi kuonekana kwa macho ya kawaida. Harakaharaka nikawa nawafuata wale manesi na madaktari kule walikokuwa wanaelekea kwa lengo la kwenda kuona kinachojadiliwa.
Cha ajabu zaidi, nilipofika kwenye mlango wa kuingilia kwenye ule ukumbi, nilimkuta yule mwanamke, mama yake mdogo Shamila naye akiwa ameshafika, nikamtazama nikiamini yeye hawezi kuniona. Cha ajabu na yeye aligeuka haraka na kunikazia macho, tukawa tunatazamana.
Nilijifunza kitu kingine kwamba kumbe ukiwa katika hali ambayo huwezi kuonekana kwa macho ya kawaida, akija mtu mwingine ambaye naye anakuwa kwenye hali kama yako, mnaweza kuonana vizuri, yaani yeye akakuona na wewe ukamuona ingawa watu wengine wa pembeni wanakua hawana uwezo wa kumuona yeyote kati yenu.
Alinisogelea na kunigusa, kingine cha ajabu ni kwamba nilihisi kabisa kwamba nimeguswa na mtu, akanivutia pembeni na kuanza kuzungumza na mimi kwa sauti ya chini, akaniambia Shamila yuko ndani na amewekwa chini ya ulinzi, amejaribu kumtorosha lakini ameshindwa peke yake, akaniomba tukaunganishe nguvu ili tumtoe haraka iwezekanavyo.
“Sasa tutafanyaje” nilimuuliza huku hofu ikianza kuniingia kwani kwa mbali niliwaona askari wengine wawili wenye silaha wakija, akaniambia tukiingia niwe namfuatisha kila anachokifanya, nikatingisha kichwa kuonesha kukubaliana naye. Akaniminya mkono na kunitazama usoni, akaniambia natakiwa niishinde hofu ndani ya moyo wangu. Nadhani aliniona jinsi nilivyoanza kuingiwa na wasiwasi, nikatingisha tena kichwa.
Pale kwenye geti la kuingilia, alinionesha ishara kwamba tunatakiwa kuingia kinyumenyume, tukafanya hivyo na muda mfupi baadaye tayari tulikuwa ndani. Madaktari na manesi walikuwa tayari wameshakaa kwenye nafasi zao huku wengine wakiendelea kuingia.
Mbele kabisa kulikuwa na meza kuu ambako walikuwa wamekaa watu walioonesha kuwa viongozi wa juu wa hospitali hiyo pamoja na askari aliyekuwa na nyota nyingi mabegani, nadhani alikuwa ni kiongozi wa polisi.
Upande wa kushoto, alikuwa amekaa Shamila huku amezungukwa na askari wawili wa kike, mmoja kila upande. Pembeni kidogo, walikuwa wamekaa wale walinzi tuliowapita getini usiku wakati tukitoroka, ambao nao ilionesha wamewekwa chini ya ulinzi. Tulipita mpaka mbele kabisa huku mtu yeyote akiwa hatuoni.
Akanipa ishara kwamba tunatakiwa kuwazunguka wale askari waliokuwa wamemuweka chini ya ulinzi Shamila mara saba kwa uelekeo tofauti, yaani mimi nianzie kulia kwenda kushoto na yeye kushoto kwenda kulia.
Tulianza kufanya kazi hiyo huku kukiwa hakuna mtu yeyote aliyekuwa akielewa kinachoendelea. Tulizunguka mzunguko wa kwanza, wa pili na hatimaye mizunguko saba ilitimia, akanionesha ishara kwamba inatakiwa tuwaguse vichwani wale askari, kweli tulifanya hivyo.
Katika hali ambayo sikuitegemea, nilishangaa kuwaona wale askari wawili wa kike, wote wakishikwa na usingizi wa ghafla, Shamila naye akawageukia mmoja baada ya mwingine, akashangaa akiwa haelewi chochote kinachoendelea.
Wakati hayo yakiendelea, pale meza kuu daktari mmoja alikuwa akizungumza kwa kutumia kipaza sauti, akielezea jinsi tukio la kutoroshwa wagonjwa wawili lilivyofanyika usiku.
Hatukuwa na muda wa kupoteza, alionesha ishara kwamba tukamshike Shamila, mmoja kwenye bega la kushoto na mwingine bega la kulia, tukafanya hivyo kisha akanionesha ishara kwamba akihesabu mpaka tatu, tupige mguu wa kushoto chini kwa nguvu na kufumba macho na nisifumbue mpaka atakaponiambia.
Akaanza kuhesabu, moja! Mbili! Taaatu, nikakanyaga mguu wangu wa kushoto chini kwa nguvu, sawasawa na yeye, mara umeme ukakatika jengo zima, nikafumba macho kama alivyoniambia huku nikiwa nimemshikilia Shamila kwa nguvu, nikahisi kama tumezolewa na kimbunga chenye nguvu kubwa.
“Fumbua macho,” alisema, nilipofumbua macho, sikuamini nilichokiona. Tulikuwa tumerejea ndani ya kile chumba tulichokuwemo mwanzo lakini tofauti na awali, safari hii kila mmoja alikuwa amelala sakafuni, kuanzia mimi, yule mwanamke, Raya na Firyaal huku akiwa ameongezeka mtu mwingine kati yetu, Shamila.
Bado wale wenzetu wote walikuwa kama wamepitiwa na usingizi mzito isipokuwa mimi na yule mwanamke pekee, nikajivutavuta na kuinuka pale nilipokuwa nimelala, nikashangaa mwili wangu ukiwa umechoka kupita kiasi huku viungo vyote vikiniuma.
Yule mwanamke naye aliinuka na kukaa kwa kujiegemeza ukutani, naye akionesha kuchoka kuliko kawaida.
“Kweli wewe ni mwanaume wa shoka, njoo nikupongeze,” alisema kwa sauti ya kichovu, nikajikokota na kusimama, nikasogea mpaka pale alipokuwa amekaa, akanionesha ishara kwamba nikae chini pembeni yake, nikafanya hivyo huku sote macho yetu yakiwa kwa Shamila.
“Sikuwahi kudhani kwamba unaweza kuwa na nguvu kubwa kiasi hicho, hongera sana, utanifaa sana wewe,” alisema huku akipitisha mkono wake mmoja begani kwangu kichovu kisha akanigeukia, tukawa tunatazamana. Katika hali ambayo sikuitegemea hata kidogo, nilishangaa yule mwanamke akinibusu, tena mdomoni, nikashtuka mno.
“Hongera sana, ila inabidi upunguze mambo ya wanawake, utakuwa na nguvu zaidi ya hizi ulizonazo,” aliniambia huku akinitazama usoni.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue au bofya Simulizi za Majonzi kusoma mwendelezo.

THE GRAVES OF THE INNOCENTS (MAKABURI YA WASIO NA HATIA)- 53


ILIPOISHIA:
“Kwa nini unanifanyia hivi Togo? Ina maana nimekosea kukupenda?” alisema huku machozi yakizidi kumtoka, nikaanza kumbembeleza huku nikimfuta machozi, nikimchombeza kwa maneno matamu, zoezi hilo lilienda sambamba na kupashana misuli, tayari kwa mpambano wa kukata na mundu.
SASA ENDELEA…
Sijui baba alijuaje kinachotaka kufanyika kule chumbani kwani wakati tukiwa kwenye maandalizi ya mwishomwisho kuelekea kwenye mpambano huo wa kirafiki, kila timu ikiwa imekamia mchezo, tulishtuka baada ya kusikia mlango ukigongwa kwa nguvu, Rahma akakurupuka na kuvaa nguo zake harakaharaka, mlango ukawa unaendelea kugongwa kwa nguvu.
Ilibidi na mimi nivae zangu na kwenda kufungua, baba akaingia mzimamzima akiwa ameongozana na baba yake Rahma.
“Kuna nini kinachoendelea hapa,” baba aliuliza huku akitazama huku na kule. Hali aliyoikuta mle ndani, ilitosha kutoa majibu juu ya kilichokuwa kikitaka kufanyika, nikavaa sura ya ‘ukauzu’ na kumjibu:
“Rahma alikuwa ananitoa miiba miguuni.”
“Miba gani?” baba aliniuliza kwa ukali, ikabidi niinue nyayo zangu na kumuonesha, wote wawili wakanisogelea na kuanza kunitazama kwa makini. Niliona wametazamana kisha wakapeana kama ishara fulani.
“Rahma nenda kwa wenzako jikoni, kesi yako itaamuliwa na mama zako,” baba yake Rahma alisema kwa sauti ya chini, harakaharaka Rahma akasimama na kutoka, huku akionesha dhahiri jinsi alivyokuwa na hofu ndani ya moyo wake.
“Najua unampenda binti yangu Togo, lakini nakuomba sana mwanangu, ukifanya naye mapenzi tutampoteza, yeye si miongoni mwa jamii yetu na mwili wake hauna kinga yoyote, hebu zingatia sana ninachokwambia, nakuomba usimguse,” baba yake Rahma alizungumza kwa sauti ya chini lakini yenye msisitizo mkubwa.
Tofauti na baba ambaye kila akiongea alikuwa akifokafoka, baba Rahma alikuwa akizungumza kwa utaratibu sana na nikajikuta nikimuelewa sana.
Jambo ambalo nilishindwa kulikataa ndani ya moyo wangu ni kwamba nilikuwa nikimpenda sana Rahma kwa hiyo akili za harakaharaka zilianza kunituma kufikiria namna ninavyoweza kukivuka kikwazo kilichokuwepo kati yetu kwani kiukweli sikuwa tayari kumpoteza.
“Kwa hiyo na yeye akiwa miongoni mwetu tutaruhusiwa kuoana?” niliuliza swali ambalo liliwafanya baba na baba Rahma watazamane kwa sekunde kadhaa.
“Lakini si unajua kwamba mwenzako anasoma na siku chache zilizopita mama yake alikuwa akifuatilia mambo ya chuo?”
“Hata akimaliza hakuna shida,” nilijibu huku nikiwa na wasiwasi na atakachokisema baba.
“Wewe mtoto mpumbavu sana, yaani umeshupalia kabisa, ina maana hujui kama nyie mmeshakuwa ndugu? Halafu hiyo michezo ya mapenzi umeianza lini wakati wewe bado mdogo?”
“Lakini baba mimi nampenda Rahma.”
“Unampenda? Unajua maana ya kupenda wewe? Toka lini wewe ukampenda mtu? Hebu toa wendawazimu wako hapa, yaani badala uelekeze nguvu kwenye ulimwengu mpya tuliokufunulia unaanza mambo yako ya mapenzi hapa, una akili wewe?” baba alinifokea.
“Hapana, huna haja ya kuwa mkali mzee mwenzangu,” baba yake Rahma alimkatisha baba kisha akanisogelea pale nilipokuwa nimekaa.
“Unampenda kwa kiasi gani?”
“Nampenda sana baba.”
“Lakini nyie mmeshakuwa ndugu?”
“Mbona undugu wetu siyo wa damu?”
“Kama kweli unampenda, nakuomba uzingatie nilichokwambia, hayo mengine tuachieni sisi wazazi wenu,” baba yake Rahma alisema kwa upole. Ilihitaji ujasiri mkubwa kuzungumza mambo yale mbele ya baba lakini kwa kuwa baba Rahma alikuwa mwelewa, na mimi nilijikuta nikipata nguvu.
Majibu aliyonipa, yaliufanya moyo wangu ufurahi sana, nikajiapiza kwamba sitakutana naye tena kimwili kwa kuhofia kumpoteza lakini nikawa nafikiria mbinu nyingine mbadala na harakaharaka akili zangu zilinituma kutafuta muda wa kutosha wa kukaa na Rahma na kumweleza ukweli kuhusu mimi, baba na baba yake na mwisho nimshawishi na yeye ajiunge kwenye jamii yetu.
Tayari nilishaanza kuona dalili za ushindi, tabasamu pana likachanua kwenye uso wangu, hisia tamu zikawa zinapita kwenye mishipa yangu huku nikivuta picha ya miaka kadhaa baadaye, nikiishi na Rahma kama mume na mke halali.
“Kilichotuleta hapa siyo hiki tulichokuwa tunakizungumza,” baba yake Rahma alivunja ukimya, baba akawa anatingisha kichwa kukubaliana naye huku akiwa amenitolea macho ya ukali.
“Leo umefanya kitu cha ajabu sana na kama isingekuwa nguvu za ziada kutumika, ungeweza hata kuuawa kule Mlandizi, kama hiyo haitoshi umesababisha majanga mengine ambayo hayakuwepo kwenye ratiba, umesababisha yule dereva wa bodaboda amepoteza maisha,” alisema baba yake Rahma, kauli ambayo ilinishtua kuliko kawaida.
Kilichonishtua zaidi ni kusikia kwamba yule dereva wa bodaboda amekufa, moyo ulishtuka kuliko kawaida.
“Kibaya zaidi umesababisha watu hapa mtaani waanze kututilia mashaka, kwa nini umeenda kumroga huyo kijana dereva wa Bajaj hapo nje? Hujui kama ni hatari sana watu kujua kama unajishughulisha na haya mambo ya giza? Mtoto mpumbavu sana wewe,” baba aliongezea kwa ukali, nikajiinamia kwani kiukweli nilikuwa nimefanya makosa makubwa.
“Lakini nilikuwa nataka kujifunza,” nilijibu kwa sauti ya chini, baba yake Rahma akaniambia kwamba mambo hayo huwa hujifunzi kama unavyojifunza mambo mengine, bali kuna utaratibu wake.
Akaniambia kwamba nilichokifanya kilikuwa makosa makubwa kwa watu wa jamii yetu na kama zilivyo sheria, yeyote anayeenda kinyume lazima akumbane na rungu la Mkuu. Kauli hiyo ilizidi kunitisha moyoni mwangu, nikajaribu kuvuta taswira ya Mkuu, yule kiongozi wa watu wa jamii yetu, hofu ikazidi kunijaa.
“Ili kumfurahisha, inabidi usiku wa leo ufanye juu chini nyama zipatikane, tukifika tutaenda kukuombea msamaha na kwa kuwa utakuwa na mzigo, bila shaka atakupa adhabu ndogo, kinyume na hapo anaweza hata kuamuru uliwe nyama ukiwa hai,” alisema baba yake Rahma, nikajikuta nikitokwa na kijasho chembamba.
Baba Rahma aliniona hali niliyokuwa nayo, akaniambia nisijali watanisaidia lakini kitu cha kwanza, ilikuwa ni lazima nikatoe sadaka ya kitu ninachokipenda zaidi, nje ya familia yangu.
Sikumuelewa kauli yake hiyo, akanifafanulia kwamba wanaposema kitu, kwenye imani yao wanamaanisha mtu kwa hiyo ilikuwa ni lazima nimfikirie rafiki yangu ninayempenda zaidi ambaye ndiye angetolewa kafara usiku ili mimi nisamehewe na Mkuu kwa kitendo changu cha kwenda kwenye msiba wa mtu ambaye tumemla nyama na mimi ndiye niliyesababisha kifo chake.
“Mimi sina rafiki hapa mjini, kwanza sijazoeana na mtu yeyote,” nilijitetea, baba akaniambia kwamba anawajua marafiki zangu wengi tu Chunya.
“Sasa nitaendaje Chunya?”
“Hutakiwi kuhoji kwa sababu hakuna kisichowezekana, unachotakiwa ni kututajia mtu, vinginevyo wewe ndiyo utaaliwa leo,” baba alisema, mapigo ya moyo wangu yakawa yananienda mbio kuliko kawaida.
Nimewahi kusikia kwamba wachawi huwa na kawaida ya kuwatoa kafara watu wao wa karibu na ndiyo maana watu wakishajua kwamba wewe ni mchawi wanajitenga na kukuogopa sana lakini nilikuwa naona kama ni hadithi za kufikirika tu, lakini sasa yalikuwa yamenifika.
Ni kweli nilikuwa na marafiki wengi wanaonipenda kule nyumbani Chunya lakini sikuwa tayari hata kidogo kuona mtu yeyote asiye na hatia anapatwa na matatizo kwa sababu yangu. Nilijikuta nikijilaumu sana kwa upumbavu wangu wa kutaka kwenda kujionea mwenyewe kilichotokea kule Mlandizi.
“Tunasubiri jibu lako,” baba alinizindua kutoka kwenye lindi la mawazo.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue au bofya Simulizi za Majonzi kusoma mwendelezo.

THE GRAVES OF THE INNOCENTS (MAKABURI YA WASIO NA HATIA)- 54


ILIPOISHIA:
Ni kweli nilikuwa na marafiki wengi wanaonipenda kule nyumbani Chunya lakini sikuwa tayari hata kidogo kuona mtu yeyote asiye na hatia anapatwa na matatizo kwa sababu yangu. Nilijikuta nikijilaumu sana kwa upumbavu wangu wa kutaka kwenda kujionea mwenyewe kilichotokea kule Mlandizi.
“Tunasubiri jibu lako,” baba alinizindua kutoka kwenye lindi la mawazo.
SASA ENDELEA…
“Lakini baba…”
“Lakini nini? Hakuna mjadala, kinachotakiwa hapa ni utekelezaji tu,” alisema baba na kunitishia kwamba endapo sitatoa majibu, kwa kuwa yeye anawafahamu marafiki zangu, atapendekeza jina lolote.
Kwa mara nyingine nilikuwa nimeingia kwenye mtego hatari wa kutaka kupoteza maisha ya mtu asiye na hatia kwa sababu ya uzembe wangu. Nilijisikia vibaya sana, nikashindwa kuzuia machozi yasiulowanishe uso wangu.
“Hata sisi mwanzo tulikuwa kama wewe, utazoea tu,” alisema baba yake Rahma. Sikujua ni nini hasa kilichotokea kwenye akili za baba na baba yake Rahma mpaka wachukulie kitendo cha kukatisha maisha ya mtu asiye na hatia kuwa cha kawaida kiasi kile.
Baada ya kulumbana kwa muda mrefu, baadaye niliamua kusalimu amri, nikamtaja rafiki yangu kipenzi, Sadoki. Kilichosababisha nikamchagua Sadoki, ni kwa sababu dakika za mwisho, urafiki wetu ulikuwa umeingia dosari baada ya siku moja kumkuta akishirikiana na watu wengine kumteta baba yangu kwamba alikuwa mchawi.
Kwa kipindi hicho, nilikuwa bado sijajua ukweli kwamba baba ni mchawi au mganga kwa sababu mara zote nilizokuwa namuuliza alikuwa akisema kwamba yeye ni mganga na wala si kweli kwamba anajihusisha na mambo ya kishirikina kwa hiyo yeyote niliyemsikia akizungumza mabaya ya baba, alikuwa akigeuka na kuwa adui yangu.
Siku nyingi zilikuwa zimepita tangu siku tulipotaka ‘kuzichapa’ maana baada ya kumkuta akimsema vibaya baba, nilimjia juu sana, kama isingekuwa watu wazima waliokuwa jirani nasi, huenda tungepigana na kuumizana sana.
Hata hivyo, tukio hilo moja halikuharibu ukweli kwamba tulikuwa marafiki wakubwa kwa sababu nakumbuka mara kwa mara alikuwa akija kwetu, na mimi nilikuwa nikienda kwao. Kwa kifupi ni kwamba ukiachilia mbali hiyo dosari ndogo iliyotokea, tulikuwa tumeshibana kisawasawa.
Baada ya kumtaja jina, sikuweza kuendelea kukaa mle chumbani, nilitoka na kwenda bafuni huku nikichechemea, nikajifungia na kuanza kulia kwa uchungu, baba na baba yake Rahma wakabaki chumbani kwangu wakiendelea kujadiliana mambo yao. Nililia mpaka macho yakawa mekundu kabisa, nilimuonea huruma Sadoki, nilimuonea huruma mama yake na wadogo zake.
Walikuwa wakimtegemea kwa sababu baba yao alifariki wakiwa bado wadogo kwa hiyo baada tu ya kumaliza shule ya msingi, Sadoki alikuwa akienda kufanya vibarua kwenye machimbo ya dhahabu na fedha kidogo alizokuwa akizipata ndizo zilizokuwa zikiihudumia familia yao.
Nikiwa bado naendelea kulia kule bafuni, baba alikuja kunigongea, ikabidi ninawe uso harakaharaka, nikatoka huku uso wangu nikiwa nimeuinamisha. Tulirudi chumbani kisha akaanza kunipa maelekezo kwamba usiku wa siku hiyo tunatakiwa kusafiri kuelekea Chunya.
“Tukifika, inabidi twende mpaka nyumbani kwa huyo rafiki yako, kuna dawa utaitega mlangoni, asubuhi akiwa anatoka anatakiwa airuke, akishairuka tu kazi itakuwa imekwisha.
“Sasa tutaendaje Chunya na kufanya hivyo unavyosema kabla hakujapambazuka?” niliuliza kwa sababu kama ni mabasi, muda huo tusingeweza kupata la kwenda Mbeya na hata kama lingepatikana, tusingewahi kama baba alivyokuwa anasema.
“Hutakiwi kuhoji sana, sikiliza kwa makini ninachokueleza,” baba alinikatisha, akaendelea kunipa maelezo ya namna ya kukamilisha zoezi hilo ambayo kwangu yalikuwa yakiingilia sikio la kushoto na kutokea la kulia.
Sikuona sababu yoyote ya kumuadhibu Sadoki kwa makosa ambayo nilikuwa nimeyafanya mwenyewe, nikajikuta nikijihisi hatia kubwa mno ndani ya moyo wangu. Basi tuliendelea kuzungumza pale, kisha baba akaniambia nijiandae kwa safari.
Walitoka na kuniacha nimejilaza kitandani, machozi yakaanza kunitoka tena na kwa sababu nilikuwa nimejilaza kwa kutazama juu, yalikuwa yakichuruzika kupitia kona za macho yangu mpaka kichwani na kupotelea kwenye shuka lililokuwa limetandikwa pale kitandani.
“Hivi ndiyo nimeshakuwa mchawi?” nilijiuliza swali kama mwendawazimu. Ni mimi ndiye niliyekuwa na shauku kubwa ya kuwa na nguvu zile za ajabu lakini sijui ni kutoelewa au ni kitu gani, ndani ya muda mfupi tu nilishaanza kuhisi kwamba pengine nimebeba mzigo mzito ambao sina uwezo nao. Zile kauli za baba akinikebehi kwamba bado nina akili za kitoto zikawa zinajirudia ndani ya kichwa changu.
Niliendelea kutafakari kwa kina na baadaye usingizi mzito ulinipitia, nikiwa usingizini nilianza kuota ndoto za ajabuajabu na kusababisha niwe nashtuka mara kwa mara. Baadaye ndoto hizo zisizoeleweka zilikoma, nikalala mpaka majira ya saa mbili za usiku nilipokuja kuzinduliwa na sauti ya baba aliyekuwa akiniita, nikakurupuka na kuamka.
“Umeshajiandaa?”
“Ndiyo,” nilimjibu huku nikijifikicha macho na kujinyoosha. Ukweli ni kwamba sikuwa nimejiandaa chochote.
“Haya nifuate.”
“Lakini bado sijala.”
“Utaenda kula mbele ya safari,” alisema baba huku akinihimiza nisimame. Nilishuka kitandani, miguu ikawa inauma sana hasa kwenye nyayo kutokana na majeraha ya ile miiba niliyotolewa na Rahma. Ilibidi nijikaze kisabuni kwa sababu ni mambo ambayo nilijitakia.
Tulitoka mpaka nje bila kuonekana na mtu yeyote, tukamkuta baba yake Rahma amesimama mlangoni, akionesha kwamba alikuwa akitusubiri. Alinipa kofia kubwa na kuniambia niivae, sikumuelewa kwa sababu gani amefanya vile. Tulitoka, mimi nikiwa katikati na kwenda hadi pale kwenye maegesho ya Bajaj, tukaingia kwenye mojawapo na baba yake Rahma akampa maelekezo dereva kwamba atupeleke Mwenge.
Sikuwa napajua Mwenge zaidi ya kupasikia tu, ni hapo ndipo nilipoelewa kwa nini baba yake Rahma alinipa ile kofia kwa sababu japokuwa nilikuwa nimeivaa, na kuziba sehemu kubwa ya uso wake, wale madereva Bajaj walikuwa wakinitazama kama wanaotaka kuhakikisha kama ni mimi kweli au laah!
Sikuwajali zaidi ya kuwadharau kwa sababu sasa nilikuwa na uwezo wa kumfanya mtu yeyote ninavyotaka mimi. Bajaj ilianza kukata mitaa na baada ya muda, tuliingia kwenye barabara ya lami iliyokuwa na magari mengi.
Safari ikaendelea mpaka tulipofika mahali kwenye mataa yenye mwanga mkali ambayo licha ya kwamba ilikuwa ni usiku, yalikuwa yakiangaza sehemu yote, watu wakiendelea na shughuli zao utafikiri ni mchana.
Tulishuka kwenye Bajaj huku nikishangaa huku na kule, moyoni nikawa najisemea ‘mjini kuzuri sana’. Tukaanza kuvuka barabara mbili pana ambazo katikati zimetenganishwa na bustani ya maua.
Kiukweli kama ningekuwa peke yangu, nisingeweza kuvuka kwa sababu kulikuwa na magari mengi mno, nikawa naung’ang’ania mkono wa baba Rahma maana baba naye alionesha kuwa na mchecheto.
Tulivuka salama mpaka upande wa pili ambako tulipanda magari mengine yanayoelekea Kunduchi. Kila kitu kilikuwa kigeni kwangu, safari ikaanza mpaka tulipofika Kunduchi, tukashuka kwenye gari na kuanza kutembea kwa miguu. Sikuwa najua tunaelekea wapi, baada ya muda tukatokezea kwenye makaburi yaliyokuwa karibu na bahari.
“Haya ni makaburi ya Wagiriki, ni ya zamani sana na hapa ndiyo hutumika kama njia ya kuingia na kutoka kwenda sehemu yoyote,” baba yake Rahma alinielekeza kwa sauti ya upole, tukaingia mpaka katikati kabisa ya makaburi hayo, mahali palipokuwa na mti mkubwa wa mbuyu.
“Tunaenda Chunya, hutakiwi kwenda kinyume na maelekezo tunayokupa, ukifanya uzembe tu, kitakachokutokea ni juu yako,” alisema baba kwa sauti ya msisitizo, nikawa natingisha kichwa kukubaliana naye. Tulikaa chini na kuweka kama duara hivi, tukashikana mikono kisha nikaambiwa nifumbe macho.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue au bofya Simulizi za Majonzi kusoma mwendelezo.


SEVEN DAYS IN HELL (SIKU SABA KUZIMU)- 51


ILIPOISHIA:
“Sikuwahi kudhani kwamba unaweza kuwa na nguvu kubwa kiasi hicho, hongera sana, utanifaa sana wewe,” alisema huku akipitisha mkono wake mmoja begani kwangu kichovu kisha akanigeukia, tukawa tunatazamana. Katika hali ambayo sikuitegemea hata kidogo, nilishangaa yule mwanamke akinibusu, tena mdomoni, nikashtuka mno.
“Hongera sana, ila inabidi upunguze mambo ya wanawake, utakuwa na nguvu zaidi ya hizi ulizonazo,” aliniambia huku akinitazama usoni.
SASA ENDELEA…
“Sijakuelewa,” nilimwambia, akashusha pumzi ndefu na kukaa vizuri pale juu ya zulia. Bado si Raya, Shamila wala Firyaal waliokuwa wamezinduka.
“Utanielewa tu,” inabidi kwanza tukaoge kuondoa uchovu halafu tuwasaidie na hawa nao warudi kwenye hali yao ya kawaida, tuna kazi nyingine ya kumsaidia Shenaiza, ni lazima arudiwe na fahamu zake, tena ikiwezekana haraka iwezekanavyo,” alisema mwanamke huyo kisha akapiga miayo mfululizo na kujinyoosha.
“Kwa kawaida, kila binadamu huwa anazalisha nguvu, nadhani hilo nilishakueleza kutoka mwanzo ingawa ni wachache sana wanaolitambua hili.
“Yaani ni kama kupepesa kope, unajua ni mpaka mtu akukumbushe kwamba muda wote macho yako yanapepesa kope ndiyo unakumbuka?” alisema, nikawa sioni chochote kipya kwenye mazungumzo yake kwa sababu ni jambo ambalo nilikuwa nimeshalisikia sana maishani mwangu kwamba kila binadamu anazalisha nguvu zisizoonekana.
“Nguvu tunazozalisha huwa zinatengeneza kitu kinachoitwa aura ambacho wengine huwa wanakiita ni mwili usioonekana juu ya mwili unaoonekana. Sasa kwa mtu mwenye utambuzi wa nguvu hizi, anao uwezo wa kuuona mwili huu.
“Kwa mtu ambaye anaishi maisha ya kitakatifu, yaani hanywi pombe, havuti sigara, hafanyi zinaa, hawasemi vibaya watu wengine, hana wivu wala kinyongo, ana upendo wa dhati kwa watu wote na ambaye moyo wake uko safi, hii aura huwa na kawaida ya kung’aa sana. Mtu akikutazama tu anaiona nguvu inayokuzunguka.
“Lakini vilevile kama mtu anaishi maisha ya hovyo, pengine ni mlevi sana, anafanya ngono hovyohovyo, ana wivu, hasira, vinyongo na tabia mbayambaya, kwa kawaida huwa aura yake inafifia sana na kama una utambuzi wa nguvu hizi, ukimtazama tu unamjua ndiyo maana nilikwambia vile,” alisema yule mwanamke na kuzidi kunishangaza.
Kitu alichokisema sikuwa nimewahi kukisikia sehemu yoyote, nikabaki nimepigwa na butwaa, akaendelea:
“Japokuwa watu wengi huwa hawaelewi kuhusu aura kwa hiyo hawajui umuhimu wa kuishi kitakatifu hata kama huna dini, siyo kitu cha mchezomchezo. Aura ya mtu huanza kuishi kabla mtu hajazaliwa na huendelea pia mpaka mtu anapokufa. Ndiyo maana mtoto anapokaribia kuzaliwa, tafiti zinaonesha kwamba huwa ana uwezo wa kuelewa kinachoendelea kwenye ulimwengu wa nje.
“Hii ni kwa sababu tayari mwili wake ambao hauonekani unakuwa umeshaingia kwenye ulimwengu wa kawaida. Akishazaliwa, huwa inatakiwa mwili wake halisi uungane na hii aura na hiyo hufanyika katika kipindi cha siku arobaini tangu mtoto azaliwe ndiyo maana kuna tamaduni nyingi kwamba mtoto anatakiwa kuanza kutolewa nje baada ya siku arobaini kwani pale inakuwa tayari aura yake na mwili halisi vinakuwa vimeungana hivyo anakuwa na kinga dhidi ya mambo mabaya yasiyoonekana kwenye ulimwengu wa kaiwada.
“Hiyo pia hutokea pale mtu anapokufa ambapo nafsi inapotengana na mwili, aura huwa inaendelea kuishi mpaka baada ya siku arobaini ndiyo nayo hutoweka, ndiyo maana pia huwa kuna tamaduni za kufanya arobaini ya marehemu kwani pale ndiyo uhai huwa unakuwa umefikia mwisho.”
Maelezo hayo yalinifanya nikune kichwa kwani siyo siri yalikuwa yamenichanganya sana akili. Ni mambo ambayo sikuwahi kuyasikia kabla lakini kwa jinsi alivyokuwa akiyafafanua, ilionesha dhahiri kwamba ni kweli. Hata mimi sikuwahi kupata jibu la kwa nini mtoto anatakiwa atolewe nje baada ya siku arobaini tangu azaliwe na kwa nini mtu akifa, msiba huwa unahitimishwa baada ya siku arobaini.
“Lakini mamdogo…”
“Usiniite mamdogo, ningependa zaidi uniite kwa jina langu halisi ambalo ni watu wachache huwa wanalijua. Nina majina mengi lakini jina langu halisi ni Junaitha,” alisema huku akiinuka pale alipokuwa amekaa.
“Hakuna cha lakini… punguza wanawake ili aura yako ing’ae na kukuongezea nguvu, mimi sijui nina mwaka wa ngapi simjui mwanaume,” alisema huku tayari akiwa amesimama, akanipa mkono kama ishara ya kutaka anisaidie kuinuka.
Nilibaki kumtazama tu usoni, mambo mengi yalikuwa yakipita ndani ya kichwa changu.
“Mbona unanitumbulia macho? Amka twende ukaoge, bado kuna kazi kubwa leo,” alisema yule mwanamke, nikampa mkono, akanishika na kunivuta kidogo, nikasimama.
“Halafu inatakiwa pia uwe makini na vyakula unavyokula, inaonesha mwili wako hauna uzito unaotakiwa, hata hao wanawake unaotembea nao hovyo huwa unawaridhisha kweli? Wanaume wa siku hizi wana tatizo kubwa la upungufu wa nguvu za kiume, na wewe usije kuwa miongoni mwao,” alisema huku akitabasamu.
Japokuwa mwenyewe alichukulia kama masihara lakini kwa hulka za kiume, niliona kama amenidharau sana. Maneno yake ni kama yalikuwa yakihitaji nifanye kitu fulani kumthibitishia kwamba sikuwa mtu wa mchezomchezo bali mwanaume niliyekamilika.
Nilipounganisha na tukio la yeye kunibusu kwenye midomo yangu wakati akinipongeza, akili nyingine zilianza kupita ndani ya kichwa changu.
“Kwa hiyo unaishije bila mume?”
“Kwani wewe unapata faida gani kubadilishabadilisha wanawake?” aliniuliza swali juu ya swali ambalo lilinifanya nijiulize sana kwa nini alikuwa akinikomalia kuhusu suala la mimi kuwa na wanawake wengi. Elimu aliyonipa ilikuwa imetosha kunifanya nijitambue lakini kwa nini alikuwa akiendelea kuulizauliza kuhusu mimi kuwa na wanawake? Sikupata majibu.
“Mbona unakuwa mkali sana kwangu Junaitha? Au kuna kitu nimekuudhi?”
“Ndiyo umeniudhi, kwa nini kijana mtanashati kama wewe usitafute mwanamke mmoja tu anayejitambua ukatulia naye?” nilijikuta nikishindwa kujizuia, nikaangua kicheko kwani tayari nilishaanza kupata picha ya kilichokuwa kikiendelea ndani ya kichwa chake.
“Kwa hiyo unanidharau si ndiyo? Yaani mi naongea mambo ya maana wewe unacheka,” alisema, akatoka na kuniacha nimesimama palepale, nikiwaangalia wale waliokuwa wamelala juu ya zulia, kila mmoja akiwa hajitambui kwa uchovu.
“Hebu njoo huku,” nilisikia sauti ya Junaitha ikitokea chumbani kwake, harakaharaka nikatoka pale na kuelekea kule sauti ilikokuwa inatokea.
“Ingia tu mlango upo wazi,” alisema, nikageuka huku na kule kwanza kwa sababu sikuona kama ni heshima kwa mtoto wa kiume kuingia chumbani kwake, hasa ukizingatia ukweli kwamba alikuwa amenizidi sana umri. Nikapiga moyo konde na kuingia ndani ya chumba hicho cha kisasa kilichokuwa na vitu vingi vya thamani.
“Chukua taulo pale kabatini ingia bafuni ukaoge,” alisema akiwa amekaa juu ya kitanda kikubwa cha kisasa akihangaika kufungua zipu ya gauni alilokuwa amevaa, nikaelekea pale kwenye kabati aliponielekeza, nikachukua taulo na kuanza kuelekea kwenye lile bafu la ndani kwa ndani kule chumbani kwake.
Nililazimika kuingia na nguo zote bafuni kwani nilikuwa naona aibu kuvua hata shati mbele ya macho yake.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.
Je, nini kitafuatia? Usikose next issue au bofya Simulizi za Majonzi kusoma mwendelezo.