Sunday, December 31, 2017

Yanga SC yafunga mwaka kwa aibu, Yanduwazwa na Mbao FC


Klabu ya Yanga imefunga mwaka 2017 kwa kipigo kitakatifu kutoka kwa klabu ya Mbao FC ya jijini Mwanza kwenye mchezo wa mzunguuko wa 12 wa Ligi Kuu Vodacom Tanzania Bara.

Kipigo hicho cha magoli mawili nunge kimewafanya wasalie kwenye nafasi ya tatu ya msimamo wa Ligi Kuu ambapo mahasimu wao Simba SC ndio vinara mpaka sasa.

Magoli yote ya Mbao FC yamefungwa na Habib Kiyombo kunako dakika ya 53 na 68 ya mchezo huo uliyokuwa na msisimko wa hali ya juu.



No comments:

Post a Comment