Friday, December 29, 2017

Israel kukipa kituo cha treni jina la Trump



Waziri wa uchukuzi nchini Israel,Yisrael Katz ametaka kuchimbwa kwa reli ya chini kwa chini kwenye mji wa zamani wa Jerusalem karibu na ukuta wa Magharibi na kupewa jina la Donald Trump.

Yisrael Katz alisema kuwa anataka kumpa heshima Rais huyo wa Marekani kufuatia uamuzi wake wa kutambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel.

Reli hiyo mpya ya chini na kituo cha treni ni sehemu ya mradi wa reli ya mwendo kasi kutoka Tel Aviv inatarajiwa kuzinduliwa mwaka ujao.

Bw. Katz aliliambia gazeti moja la Israel la Yedioth Ahronoth kuwa kuongezwa kwa reli kutoka Tel Aviv kwenda Jerusalem ndio mradi muhimu zaidi kwa wizara ya uchukuzi.

No comments:

Post a Comment