Sunday, December 31, 2017

Nikki wa Pili afunguka kuhusu Muziki wa Hip Hop



Msanii wa Hip Hop kutoka Weusi Kampuni, Nikki wa Pili amesema muziki wa sasa wa Hip Hop ushindani wake upo kibiashara zaidi kwa kuangalia jinsi ya kuwakonga mashabiki jukwaani na namna ya msanii mwenyewe anavyoweza kujiweka kibiashara.

Nikki wa Pili amedai kuwa kinachoangaliwa kwa sasa ni kuuza bidhaa yako na bidhaa nzuri ndiyo inayouza sokoni kwa hiyo ndio muziki wa Hip Hop ya sasa ulivyo.

Akizungumzia ushindani wa Hip Hop ulivyo wa kibiashara, Nikki wa Pili amesema ni ushindani ambao Msanii mwenzako akitoa video kali na wewe unatoa video kali zaidi au akifanya show nzuri na wewe unafanya show kali zaidi yake. Msikilize Nikki wa Pili kwenye mahojiano yake na Bongo5 hapa chini





No comments:

Post a Comment