Sunday, December 31, 2017

"Bora wafute vyama vingi" - Mbowe


Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe amefunguka na kusema kama Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na serikali haioni umuhimu na uwepo wa vyama vingi nchini watumie uwingi wao bungeni wavifute vyama hivyo.

Mbowe amesema hayo leo wakati akiongea na waandishi wa habari na kusema toka imeingia madarakani Serikali ya awamu ya tano watu wa upinzani wanaonekana ni maadui

"Tumemwambia Rais mara nyingi na chama chake kama wao wanaamini upinzani ni hasara kwa nchi na hawajaweza kuona faidi ya vyama vingi vya siasa, kama Chama Cha Mapinduzi hakijaona umuhimu vyama vingi vya siasa kwenye nchi hii kwa miaka 25 hii wana wingi wa kutosha bungeni ni bora wafute vyama vingi lakini ku pretend tupo kwenye vyama vingi wakati mnavikandamiza na kuvifunga mikono wakati nyinyi mnafanya siasa wenzenu wasifanye siasa" alisema Mbowe

Mbali na hilo Mbowe amesema kuwa kupitia chama chake cha CHADEMA kwa mwaka 2018 watakuwa na kazi ya kupigania mchakato wa Katiba Mpya pamoja Tume Huru ya Uchaguzi na kusema hilo wanaliweka wazi mapema ili ifahamike.


No comments:

Post a Comment