Sunday, December 31, 2017

TOP 10: Stori 10 za michezo za kukumbukwa 2017


TOP 10: Stori 10 za michezo za kukumbukwa 2017

Sababu za RC Geita kuzuia likizo kwa watumishi


Sababu za RC Geita kuzuia likizo kwa watumishi


"Sio vizuri kufunua makaburi, Bukoba tumewahi poteza bilioni 18" - Meya Bukoba

"Sio vizuri kufunua makaburi, Bukoba tumewahi poteza bilioni 18" - Meya Bukoba


EXCLUSIVE: Compozers wazungumza kuhusu Alikiba na Diamond

EXCLUSIVE: Compozers wazungumza kuhusu Alikiba na Diamond


Video | Fid Q Ft Diamond Platnumz & Rayvanny – Fresh Remix | Mp4 Download

Video | Fid Q Ft Diamond Platnumz & Rayvanny – Fresh Remix | Mp4 Download


Video | Fid Q Ft Diamond Platnumz & Rayvanny – Fresh Remix | Mp4 Download

DOWNLOAD

TRA yatoa sababu ya Kakobe kuchunguzwa



Dar es Salaam. Kauli ya Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Zachary Kakobe kuwa ana fedha  nyingi kuliko Serikali imeiibua Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ambayo imetangaza kuanza mchakato wa kufuatilia ulipaji wake wa kodi.

TRA imesema uamuzi huo unatokana na kiongozi huyo wa kiroho kutokuwamo katika kumbukumbu za ulipaji kodi za mamlaka hiyo.

Na kama utajiri wake unatokana na sadaka pekee, Kamishna Mkuu wa TRA, Charles Kichere aliwaambia wanahabari jana kuwa hilo litakuwa jambo la kushtua.

Kanisa hilo kupitia kwa mtendaji kazi wake, Natus Mwita limesema litatoa ushirikiano kwa TRA japo hadi jana mchana lilikuwa halijapokea taarifa rasmi kuhusu kauli hiyo ya TRA.

Kauli ya TRA imetolewa siku tatu tangu kusambaa kwa picha za video zikimuonyesha Askofu Kakobe akiwa katika mahubiri kwenye kanisa lake lililopo Mwenge jijini Dar es Salaam, akisema  kiwango cha fedha alichonacho si tu ni zaidi ya kile cha Serikali, bali pia anaweza kuwakopesha fedha hata mawaziri.

“Mimi sihitaji hela nina hela kuliko Serikali, si unaona shughuli yenyewe hii, sio pesa hii,” alihoji akionyesha waumini waliohudhuria ibada hiyo ambao nao walisikika wakijibu, “ni pesa.”

Alisema, “Nimewaambia waandishi wa habari hakuna wa kunihonga wala kunipa hela yoyote hata waziri akiwa hana hela aje kwangu nitamkopesha. Lakini neno  hili lazima litapelekwa vilevile lilivyo. Mtawala akifanya dhambi, atajulishwa dhambi yake, hapa umekengeuka, hapa si njia upasayo kuiendea, njia ya kuiendea ni hii.”

Kwa taarifa hiyo ya ukwasi wa Askofu Kakobe, Kamishna Kichere alisema mamlaka hiyo imeipokea kwa furaha na inataka kujiridhisha juu ya vyanzo vyake.

Alibainisha kuwa TRA inafahamu kuwa shughuli za kidini hazitozwi kodi lakini inataka kufahamu kama fedha hizo za Askofu Kakobe zinatokana na sadaka pekee au kuna shughuli nyingine za kiuchumi.

“Tumefuatilia hakuna kumbukumbu za Askofu Kakobe kulipa kodi, sasa tumeona tumfuate ili maofisa wetu wakajiridhishe kama fedha hizo anazozizungumzia zinatokana na sadaka,” alisema.

“Na kama hana shughuli zozote za kiuchumi ikiwa ina maana utajiri huo unatokana na sadaka ni jambo la kushtua kidogo lakini sisi tutaishia hapo.”

Alisema, katika taarifa za mamlaka hiyo wapo watu wengi wenye fedha nyingi na kumbukumbu zao za kodi zipo lakini Askofu Kakobe si miongoni mwao.

Alimwomba Askofu Kakobe kutoa ushirikiano kwa maofisa wa TRA watakaomtembelea kwa ajili ya ukaguzi.

Alipoulizwa kwa nini uhakiki ufanyike sasa na si miaka ya nyuma, Kichere alisema ni baada ya kusikia kwamba ana fedha nyingi kuliko Serikali wakati anafahamika kuwa ni kiongozi wa taasisi ya dini.

Askofu Kakobe alitoa kauli hiyo siku moja baada ya viongozi wengine wa dini kutumia mkesha na ibada ya Sikukuu ya Krismasi kuhimiza amani, upendo, kukemea maovu,  kushauri viongozi wa Serikali kukubali kushauriwa na kutominya uhuru wa watu kutoa maoni.

Wakati maoni ya viongozi hao wa dini akiwamo Askofu Kakobe yakigeuka kuwa mjadala, Serikali kupitia kwa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali mstaafu Projest Rwegasira ilitoa taarifa ikiwataka viongozi hao kutojihusisha na masuala ya siasa, bali wajikite kuzungumzia mambo yanayoendana na malengo ya kuanzishwa kwa taasisi zao, vinginevyo zitafutwa.

Meja Jenerali Rwegasira alisema viongozi wa dini wanapaswa kujikita kuzungumzia masuala ya dini yanayoendana na malengo ya kuanzishwa kwa taasisi zao na kuachana na ya kisiasa.

Alisema ukiukwaji wowote wa sheria ni kosa linaloweza kusababisha jumuiya husika kufutiwa usajili kama ilivyoelezwa kwenye kifungu cha 17 cha sheria husika.

Hata hivyo, juzi katibu mkuu huyo alisema viongozi hao wa dini wakiisifia Serikali au viongozi wake hawatakuwa wametenda kosa lolote.

Mbali na kuzungumza katika ibada hizo, baadhi ya viongozi hao walitumia mitandao ya kijamii kueleza mambo yanayofanana na hayo.

Miongoni mwao ni Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Karagwe mkoani Kagera, Benson Bagonza ambaye alitumia ukurasa wake wa mtandao wa Facebook kuhoji mipaka ya kuzungumzia masuala ya dini na siasa, huku akitaka wananchi kutojengewa hofu ya kutoa maoni yao.

Jana alipoulizwa kuhusu ujumbe mwingine alioutuma katika mtandao huo alisema, “Kwa hiki kinachoendelea sasa, suluhu ni kufanyika kwa mjadala wa kitaifa ili kuwekana sawa.

“Anayezuia watu kuzungumzia siasa huyu anayezuia atakuwa hana historia vizuri, wakati wa Bunge la Katiba, kulikuwa na wawakilishi wa dini tena na wapiga ramli walikuwemo. Kama walitambuliwa na kushirikishwa katika kuandaa Katiba inakuwaje useme tusizungumze siasa, kama tuliingizwa Bunge la Katiba kwa nini sasa tunazuiwa kuzungumza,” alihoji.

Alisema, “Amri za kibabe au nguvu kwa viongozi wa dini sidhani kama zinajenga. Kuna viongozi wa dini wanaona wanajua siasa kuliko wanasiasa na kuna wanasiasa wanaona wanajua dini kuliko viongozi wa dini, ndiyo maana nikasema mjadala wa kitaifa unahitajika.”

Kamishna wa Magereza azungumzia msongamano wa wafungwa



Mbeya. Kamishna Jenerali wa Magereza, Juma Malewa amesema jeshi hilo linakabiliwa na msongamano wa wafungwa kutokana na kuongezeka vitendo vya uhalifu na makosa ya kijinai.

Dk Malewa amesema hayo leo Jumapili Desemba 31,2017 katika Gereza Kuu la Mkoa wa Mbeya akiwa ziarani kukagua magereza na kuzungumza na askari wa jeshi hilo.

Amesema msongamano unatokana na majengo yanayotumika kuwahifadhi wafungwa ni yaliyojengwa enzi za mkoloni.

Hata hivyo, amesema wamejipanga kuendelea kuongeza idadi ya magereza kwa kila wilaya licha ya baadhi ya wananchi kutopendezewa na jambo hilo.

“Wakati tunapata Uhuru watu tulikuwa kama 10 milioni, hadi sasa majengo kama yameongezeka basi ni mawili lakini ni yaleyale; pia kuna makosa mapya ya uhalifu yameongeza ambayo zamani hayakuwepo,” amesema.

Amesema makosa ya dawa za kulevya na utakatishaji fedha yamejitokeza; huku mauaji yakiongezeka.

Pia, amesema msongamano unasababishwa na kesi zinavyoendeshwa mahakamani ambako zipo zinazochukua muda mrefu upelelezi kukamilika.

Wakati huohuo, Dk Malewa amesema katika kutekeleza agizo la Rais John Magufuli la kuongeza uzalishaji wa chakula kwa lengo la kujitegemea ifikapo mwaka 2022 wametenga magereza 10 yatakayotekeleza mpango wa uzalishaji.

Amesema chakula kitakachozalishwa kitatumika ndani ya magereza hayo na kulisha Taifa litakapokabiliwa na uhaba.

“Kwa sasa Jeshi la Magereza linaitegemea Serikali kwa asilimia 100 ilhali ina rasilimali watu ya kutosha kuzalisha chakula. Hivyo, tumeanza utekezaji kwa magereza 10 na lengo ni hadi kufika miaka mitano ijayo tuwe tunajitegemea kwa asilimia 100 bila Serikali,” alisema Dk Malewa.


Kanisa Katoliki yaitisha maandamano ya amani Kongo



Kuna wasi wasi wa kukosekana utulivu katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo inayokabiliwa kwa sasa na mgogoro wa kisiasa kufuatia kanisa Katoliki lenye ushawishi mkubwa nchini humo kuitisha maandamano ya amani.

Kabila ambaye waandaaji wa maandamano hayo wanamtaka atamke wazi kuwa hatawania muhula wa tatu wa uongozi, amekuwa madarakani tangu mwaka 2001 wakati aliposhika madaraka ya urais baada ya baba yake Laurent Kabila kuuawa.

Kabila alikataa kujiuzulu bada ya kumalizika  kipindi chake cha pili na cha mwisho  Desemba 2016 hatua iliyosababisha maandamano pamoja na machafuko.

Tangu kipindi hicho maanadamano yamekuwa yakipigwa marufuku licha ya wakati mwingine waandamanaji kukiuka amri ya serikali na kuendelea na maandamano hali ambayo pia imekuwa ikisababisha umwagaji wa damu.

Hatua ya kanisa Katoliki kuitisha maandamano  ya leo Jumapili licha ya serikali kuyazuia yasifanyike inawafanya baadhi ya wachambuzi kuonya juu ya uwezekano wa kukosekana utulivu.

“Maandamano ya leo Jumapili nchini Kongo yanaweza kuwa makubwa zaidi kuliko yale ya mwaka jana” ameandika kupitia ukurasa wa twitter Jason Stearns  mchambuzi aliyebobea katika masuala ya siasa za Kongo kutoka chuo kikuu cha New York kinachohusika na mahusiano ya kimataifa.

Anasema vyama vyote vikubwa vya upinzani, asasi za kiraia, makundi ya vijana wanaharakati pamoja na kanisa Katoliki yanaunga mkono maandamano hayo ya leo Jumapili.

Uchaguzi ulipaswa kufanyika mwaka huu

Uchaguzi ulikuwa ufanyike mwishoni mwa mwaka huu chini ya makubaliano yaliyoasimamiwa na kanisa  katika juhudi za kuzuia machafuko kwenye  taifa hilo kubwa lenye utajiri wa madini ambalo halijawahi kushuhudia mabadilishano ya madaraka kwa njia ya amani tangu lijipazie uhuru wake kutoka Ubeligiji mwaka 1960.

Baada ya kuahilishwa mara kadhaa hasa kutokana na vurugu katika mkoa wa  Kasai  uchaguzi huo uliocheleweshwa sasa umepangwa kufanyika  Desemba 23, mwakani.

Kiasi ya makanisa 150 ya kanisa Katoliki yametoa mwito kwa waumini wao kuitikia wito wa kuandamana  leo Jumapili mjini Kinshasa  wakiwa na biblia mkononi ili kushinikiza kutekelezwa kwa makubaliano yaliyotiwa saini mwaka mmoja uliopita  yaliyokuwa na lengo la  kurejesha uthabiti nchini humo ikiwa ni pamoja na kumtaka Kabila kuondoka madarakani.

Si baraza la maaskofu nchini humo au mwakilishi wa serikali ya mjini Vatican  amezungumzia lolote kuhusiana na maandamano hayo.

Gavana wa mji huo Andre Kimbuta wenye watu milioni 10 amesema jana Jumamosi kuwa maandamano hayo  yasiyo na kibali hayawezi kuendelea kwa maelezo kuwa mji huo hauna maafisa wa polisi wa kutosha kusimamia maandamano  ya leo.

Hata hivyo msemaji wa waratibu wa maandamano  Leonie Kandolo alisisitiza kuwa licha ya kauli hiyo ya serikali maandamano ya leo yatafanyika na kuwa maafisa wa mji huo pamoja na polisi wanalazimika kutimiza wajibu wao kuwalinda raia na mali zao.

Waandaaji wa maanadamano  wametoa mwito kwa waumini kukusanyika baada ya misa ya asubuhi kwa ajili ya kushiriki maandamano leo.

Katiba ya Kongo inamzuia Kabila kuwania muhula wa tatu wa uongozi lakini makubaliano yaliyofikiwa yanamruhusu kusalia madarakani hadi uchaguzi mwingine utakapofanyika.

Nikki wa Pili afunguka kuhusu Muziki wa Hip Hop



Msanii wa Hip Hop kutoka Weusi Kampuni, Nikki wa Pili amesema muziki wa sasa wa Hip Hop ushindani wake upo kibiashara zaidi kwa kuangalia jinsi ya kuwakonga mashabiki jukwaani na namna ya msanii mwenyewe anavyoweza kujiweka kibiashara.

Nikki wa Pili amedai kuwa kinachoangaliwa kwa sasa ni kuuza bidhaa yako na bidhaa nzuri ndiyo inayouza sokoni kwa hiyo ndio muziki wa Hip Hop ya sasa ulivyo.

Akizungumzia ushindani wa Hip Hop ulivyo wa kibiashara, Nikki wa Pili amesema ni ushindani ambao Msanii mwenzako akitoa video kali na wewe unatoa video kali zaidi au akifanya show nzuri na wewe unafanya show kali zaidi yake. Msikilize Nikki wa Pili kwenye mahojiano yake na Bongo5 hapa chini





Nape azungumzia kupokewa wanaohama vyama


Dar es Salaam. Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye amehoji sababu za vyama vya siasa kuhangaika kupokea wanachama wa vyama vingine, badala ya kushughulika na Watanzania wasio na vyama.

Akizungumza leo Jumapili Desemba 31,2017 katika mahojiano na kituo cha televisheni cha Azam, Nape amesema siku zote amekuwa na msimamo tofauti na wanachama wanaovihama vyama vyao kwa maelezo kuwa unawajenga wanaohama, si vyama.

"Kama tunataka kujenga vyama viwe vya kitaasisi ni lazima kuhamahama lisiwe suala la kawaida. Yaani mtu mpaka anahama watu waseme kweli huyu alistahili kuhama," amesema Nape.

Amesema, "Watanzania wapo zaidi ya 50 milioni, wenye uwezo wa kujiunga na vyama kikatiba wanaweza kuwa zaidi ya 30 milioni, waliopo kwenye vyama wanaweza wasifike 10 milioni. Kwa nini tunakwenda kuhangaika na wanachama wa vyama vingine badala ya kushughulika na Watanzania wasio na vyama. Tushughulike kuwashawishi hawa."

Katika kipindi hicho, mwenyekiti wa kamati ya uongozi ya Chama cha Wananchi (CUF), Julius Mtatiro na mwanahabari mkongwe, Dk Gideon Shoo waliungana na Nape kukosoa vitendo vya wanachama kuvihama vyama vyao.



Rais Karia aguswa na msiba wa Mwandishi



Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia amepokea kwa masikitiko na majonzi makubwa taarifa za kifo cha Mtangazaji wa Kituo cha Radio Uhuru, Limonga Justin Limonga.

Msiba huo wa mwanahabari mwandamizi umetokea leo Desemba 31, 2017 kwenye Hospitali ya TMJ, Mikocheni jijini Dar es Salaam.

Kutokana na msiba huo, Rais Karia ametuma salamu za rambirambi kwa Mkurugenzi wa Kituo hicho cha Radio, Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo (TASWA) pamoja na wanafamilia wote wa mpira wa miguu.

''Natambua mchango wa Limonga katika kupasha habari za michezo kupitia Radio'', amesema Karia.

Aidha Karia ameongeza kuwa hatuna budi kuwa na imani kama maandiko yanavyosema kwamba Bwana ametoa na bwana  ametwaa jina lake lihimidiwe.

"Bora wafute vyama vingi" - Mbowe


Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe amefunguka na kusema kama Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na serikali haioni umuhimu na uwepo wa vyama vingi nchini watumie uwingi wao bungeni wavifute vyama hivyo.

Mbowe amesema hayo leo wakati akiongea na waandishi wa habari na kusema toka imeingia madarakani Serikali ya awamu ya tano watu wa upinzani wanaonekana ni maadui

"Tumemwambia Rais mara nyingi na chama chake kama wao wanaamini upinzani ni hasara kwa nchi na hawajaweza kuona faidi ya vyama vingi vya siasa, kama Chama Cha Mapinduzi hakijaona umuhimu vyama vingi vya siasa kwenye nchi hii kwa miaka 25 hii wana wingi wa kutosha bungeni ni bora wafute vyama vingi lakini ku pretend tupo kwenye vyama vingi wakati mnavikandamiza na kuvifunga mikono wakati nyinyi mnafanya siasa wenzenu wasifanye siasa" alisema Mbowe

Mbali na hilo Mbowe amesema kuwa kupitia chama chake cha CHADEMA kwa mwaka 2018 watakuwa na kazi ya kupigania mchakato wa Katiba Mpya pamoja Tume Huru ya Uchaguzi na kusema hilo wanaliweka wazi mapema ili ifahamike.


Wapinzani 19 wakabidhi kadi CCM




Wanachama 19 kutoka vyama vya upinzani katika Kata za Matambarare na Mnacho wilayani Ruangwa mkoani Lindi, wamekabidhi kadi zao kwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM).

Wanachama hao kutoka vyama vya CUF na CHADEMA, wamekabidhi kadi zao kwa Waziri wakati akizungumza na wakazi wa kijiji cha Matambarare Kusini kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini hapo.

Akiwa katika kijiji cha Matambare Kusini, Waziri Mkuu amepokea wanachama 17 ambao kati yao 13 wanatoka Chama cha Wananchi (CUF) na wanne wanatoka Chama cha Maendeleo na Demokrasia (CHADEMA). Katika kijiji cha Ng’au kata ya Mnacho, Majaliwa amepokea wanachama wawili wa (CHADEMA).

Kwa upande mwingine Waziri Mkuu ambaye yupo kwenye mapumziko ya mwisho wa mwaka anaendelea na ziara ya jimboni kwake kwa kuzindua kampeni ya kitaifa ya upandaji miche bora na mipya.

Ajali mbaya ya Barabarani Kenya, Yaua watu 36 na wengine zaidi ya 11 kujeruhiwa



Watu 36 wamepoteza maisha na wengine 11 kujeruhiwa katika ajali mbaya ya barabarani nchini Kenya iliyotokea mapema usiku wa kuamkia leo.

Polisi wameeleza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni basi la abiria ambalo lilikuwa linatokea Busia mpani na nchi yaUganda lililokuwa likielekea jijini Nairobi kugongana ana kwa ana lori lililokuwa linatokea mjini Nakuru.

Mkuu wa kitengo cha trafiki katika eneo la Bonde la Ufa, Zero Arijme, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambayo amesema ilitokea saa tisa alfajiri katika barabara kuu ya kutoka Nakuru kwenda mjini Eldoret.

Kwa mujibu wa jeshi la Polisi nchini Kenya wamesema mwezi wa Desemba pekee, watu zaidi 100 wamepoteza maisha katika ajali za barabarani zilizotokea katika barabara kuu ya Nakuru kuelekea Eldoret hali ambayo inaashiria hatari kuwa katika eneo hilo ambalo limekuwa sugu kwa kutokea ajali za mara kwa mara.

Mwaka Mpya wa 2018, Watanzania wakumbushwa kudumisha amani




Katika kuelekea mwaka Mpya wa 2018 watanzania wamekumbushwa kuenzi na kudumisha Mshikamano, Amani na Upendo hususani kwa makundi ya wasiojiweza, yatima na wazee kutokana na kwamba, vitendo hivyo vimeendelea kuwa mhimili na kichocheo muhimu katika kufikia Maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini.

Haya yanajidhihirisha kwa vitendo baada ya kikosi cha Jeshi la wananchi 313 Monduli kufika katika kituo cha watoto yatima Global Cha Arusha ambapo kwa pamoja wameshiriki katika shughuli za usafi wa mazingira ya kituo hicho, kufua shuka na mablanket ya watoto lakini pia kutoa msaada wa vitu mbalimbali vyenye thamani ya shilingi milioni Tatu na fedha taslimu shilingi laki tano ikiwa ni ishara ya Upendo kwa yatima hao .

Mkurugenzi wa kituo hicho Mack Donald Kavishe anasema ni kwa mara ya kwanza kupata ugeni kama huo na kuongeza kuwa kitendo cha kushiriki usafi na kutoa msaada huo ni tiba ya kisaikolojia kwa watoto hao ili wasijisikie upweke.

Baadhi ya msaada wa vitu vilivyokabidhiwa ni Sukari, mchele, mafuta ya kujipaka na kupikia, magodoro, chumvi, vifaa vya usafi, madaftari, unga na maharagwe.

Msuva Arejea Nyumbani Kwa Mapumziko Baada Ya Kazi Nzuri Morocco




WINGA wa kimataifa wa Tanzania, Simon Happygod Msuva anatarajiwa kurejea nchini Alhamisi kwa mapumziko ya baada ya mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Morocco, maarufu kama Botola.

Akizungumza na Bin Zubeiry Sports – Online leo, Msuva amesema kwamba Ligi ya Morocco inakwenda mapumzikoni naye anarejea nyumbani kwa mapumziko na kujipanga kwa mzunguko wa pili.

“Natarajia kurudi nyumbani kuanzia Alhamisi kwa mapumziko ya baada ya mzunguko wa kwanza Ligi Kuu huku, na pia kujipanga kwa mzunguko wa pili kabla ya kurudi kambini,”amesema.

Msuva anaweza kuwa kwenye mapumziko marefu, kwa sababu michuano yote nchini Morocco sasa itasimama kupisha Fainali za Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN) zinazohusisha wachezaji wanaocheza ligi za nchini mwao pekee zinazotarajiwa kuanza Januari 13 hadi Februari 4, mwakani.

Simon Msuva (kulia) amefunga mabao matano katika mechi 13 za ligi ya Morocco na ametoa pasi za mabao matatu

Msuva anarejea nyumbani akitoka kuifungia bao pekee Difaa Hassan El-Jadidi ikishinda 1-0 dhidi ya Hassania Agadir Ijumaa.

Msuva, mchezaji wa zamani wa Yanga alifunga bao hilo dakika ya 52 katika mchezo uliofanyika Uwanja wa Ben Ahmed El Abdi mjini El Jadida, Mazghan nchini Morocco na sasa anafikisha mabao matano katika mechi 13 za ligi ya Morocco, akiwa pia ametoa pasi za mabao matatu.

Msuva anazidiwa mabao mawili mawili na Mehdi Naghmi wa Ittihad Tanger na Jalal Doudi wa Hassania Agadir wanaoongoza kwa mabao yao saba kila mmoja, wakifuiatiwa na Mouhcine Lajour wa Raja Casablanca mabao sita sawa na Bilal El Magri, Hamid Ahadad wote wa Difaa Hassan El-Jadidi na Abderrahim Makran.

Mbali na Msuva aliyewahi pia kuchezea Moro United baada ya kupita akademi ya Azam FC, mwingine mwenye mabao matano ni Badr Kachani wa Hassania Agadir.

Ikumbukwe Msuva yupo katika msimu wake wa kwanza Difaa Hassan El-Jadidi baada ya kujiunga na timu hiyo kutoka Yanga SC ya Tanzania.



Yanga SC yafunga mwaka kwa aibu, Yanduwazwa na Mbao FC


Klabu ya Yanga imefunga mwaka 2017 kwa kipigo kitakatifu kutoka kwa klabu ya Mbao FC ya jijini Mwanza kwenye mchezo wa mzunguuko wa 12 wa Ligi Kuu Vodacom Tanzania Bara.

Kipigo hicho cha magoli mawili nunge kimewafanya wasalie kwenye nafasi ya tatu ya msimamo wa Ligi Kuu ambapo mahasimu wao Simba SC ndio vinara mpaka sasa.

Magoli yote ya Mbao FC yamefungwa na Habib Kiyombo kunako dakika ya 53 na 68 ya mchezo huo uliyokuwa na msisimko wa hali ya juu.



Korea kaskazini yasema haitoacha mpango wake wa mabomu ya nyukilia



Korea Kaskazini katika salamu zake za mwisho wa mwaka imesema haitoachana na mpango wake wa silaha za nyuklia ikiwa Marekani na washirika wake wataendelea kufanya mazoezi ya kijeshi karibu na nchi yake.

Shirika la habari la Korea Kaskazini limetoa taarifa hiyo leo katika uchambuzi wake kuhusu silaha kubwa za kinyuklia zinazomilikiwa na taifa hilo pamoja na majaribio ya makombora yaliyofanywa na jeshi la nchi hiyo katika mwaka huu 2017.

Korea Kaskazini ilifanya jaribio lake kubwa la makombora mnamo mwezi Septemba na katika miezi ya Julai na Novemba ilizindua makombora matatu yenye uwezo wa kuruka kutoka bara moja hadi jingine.

Uzinduzi huo ulizusha wasiwasi kwamba huenda nchi hiyo ikawa inamiliki bomu la kinyulia linaloweza kurushwa hadi nchini Marekani na hivy kuitia hofu Marekani na kuchukua hatua za kuiwekea vikwavyo vipya katika Baraza la Uslama la Umoja wa mataifa.

Friday, December 29, 2017

VIDEO: Yanga Yafunguka Sakata La Chirwa



Klabu ya Soka ya Yanga leo imetoa ufafanuzi wa mchezaji wake Obrey Chirwa kuhusishwa kurudi kwao Zambia na kuonekana shambani akifanya shughulia za kilimo.

Akizungumza na waandishi wa habari Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Yanga Dismas Teni amesema kuwa Chirwa ni mchezaji halali wa Yanga na ni sehemu ya kikosi cha na atarejea kesho Jumamosi kuungana na wanzeke ambao wakitoka Mwanza wataelekea Zanzibar kwenye kombe la Mapinduzi ambapo kikosi hicho  kitaelekea huko hivyo .

Aidha Teni amesema kuwa kila klabu ina matatizo hivyo watu wanaongea na kundika  kwenye mitandao huwezi kuwazuia ni haki yao kufanya wanachokitaka.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI......USISAHAU KUSUBSCRIBE

WATCH HERE

Lissu aunguruma kuhusu ukiukwaji wa Haki za Binadamu



Zikiwa zimebaki siku mbili kabla ya kuuaga mwaka 2017, Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu ametoa waraka akilaani ukiukwaji wa haki za binadamu na kuminywa kwa uhuru wa kutoa mawazo.

Waraka huo alioutoa jana Alhamisi Desemba 28,2017 akiwa katika Hospitali ya Nairobi nchini Kenya anakopatiwa matibabu tangu Septemba 7,2017 aliposhambuliwa na kujeruhiwa kwa risasi kwenye makazi yake Area D mjini Dodoma.

Lissu pia amezungumzia tukio la kutoweka mwandishi wa habari wa kujitegemea wa kampuni ya Mwananchi Communications Ltd (MCL), Azory Gwanda ambaye leo ni siku ya 39 tangu alipotoweka akiwa wilayani Kibiti mkoani Pwani anakofanyia kazi zake.

“Watanzania ambao wamekuwa wakitumia uhuru wao wa maoni kutoa mawazo wamekuwa wakikamatwa na kushtakiwa mahakamani... mwanachama wa Chadema, Ben Saanane na mwandishi wa Mwananchi (Azory Gwanda) wametoweka na hawajulikani walipo. Hakuna uchunguzi au taarifa za kutoweka kwao,” amesema.

Lissu ambaye pia ni mwanasheria wa Chadema amesema vyombo vya habari  vimekuwa katika wakati mgumu baada ya kukutana na mkono wa sheria, ikiwamo kufungiwa pale vinapoandika habari zinazotafsiriwa kuwa ni za kichochezi au uongo.

Kupitia waraka huo alioupa jina ‘Barua kutoka kitanda cha Hospitali ya Nairobi’ amezungumzia pia mambo yaliyojitokeza na yanayoendelea katika kipindi cha miaka miwili ya utawala wa Serikali ya Awamu ya Tano.

Waraka huo ameutoa siku tatu baada ya kusimama kwa mara ya kwanza tangu Septemba 7,2017 aliposhambuliwa na kujeruhiwa kwa risasi.

Amesema kumekuwa na ukiukwaji wa haki za binadamu na utawala bora, huku viongozi wa upinzani na wanaharakati wakikamatwa na kuwekwa mahabusu.

Lissu amesema kutokana na watawala kuwashughulikia wanaowakosoa, uhuru wa kutoa maoni umeminya na mijadala haipo.

“Mikutano ya kisiasa imezuiwa na polisi, viongozi wanakamatwa, wabunge nikiwemo mimi (Lissu) tumekamatwa mara nyingi kwa sababu zinazohusu majukumu yetu ya kazi,” amesema.

Amesema, ‘’Hakuna njia rahisi kufikia uhuru sehemu yoyote na wengi wetu tutapitia bonde la kivuli cha kifo kabla ya kufikia mlima wa matamanio yetu.”

Pia, amevilaumu vyombo vya dola akisema tangu Septemba 7,2017 aliponusurika kuuawa akiwa eneo lenye ulinzi mpaka sasa hakuna mtuhumiwa hata mmoja anayeshikiliwa kuhusika na tukio hilo.

Kuhusu onyo la Serikali kwa viongozi wa dini kutojihusisha na masuala ya kisiasa lililotolewa jana Alhamisi Desemba 28,2017 na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Lissu amesema ni mwendelezo wa kuwazuia watu wasitumie uhuru wao kuzungumza na kukosoa.

Bashe ashauri Serikali ikubali kukosolewa


Baada ya kuwaonya viongozi wa dini wasijihusishe na masuala yaliyo nje na usajili wao, mbunge wa Nzega Mjini (CCM), Hussein Bashe ameshauri Serikali ikubali kukosolewa.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana Alhamisi Desemba 28, 2017, katibu mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Projest Rwegasira alionya kuwa Serikali inaweza kufuta usajili wa taasisi zinazokiuka sheria ya usajili wao iwapo viongozi wa dini watajihusisha na masuala tofauti na masharti ya usajili wao.

Alitoa onyo hilo baada ya viongozi wa kidini kutumia ibada za sikukuu ya Krismasi kukosoa uendeshaji wa nchi, kutaka utawala wa sheria uheshimiwe na kuhoji sababu za kuzuiwa kuzungumzia siasa.

Lakini tamko la Serikali limekosolewa na wadau, akiwemo Bashe, ambaye aliandika maoni yake katika ukurasa wa Mwananchi ulioandika taarifa ya onyo hilo.

“Kesho tutazitaka taasisi za dini zihamasishe amani, maendeleo, zipongeze ‘Its important’ (ni muhimu) kukubali kukosolewa,” ameandika Bashe katika akaunti ya Twitter.

“Gvt should not do this as far as (Serikali haipaswi kufanya hivyo kwa kuwa) hazivunji sheria. Taasisi za dini zina haki kutoa maoni yao juu ya siasa, uchumi na masuala yote ya kijamii, viongozi wa dini wana nafasi yao.”

Mwingine aliyetoa maoni ni Mathias Mushi aliyesema: ‘’Nimewaza kwa sauti kama awamu hii inathubutu kutaka kuzifuta taasisi za kidini kwa kile wanachodai kukiuka miiko na maudhui ya taasisi zao jipe adhabu wewe unayekosoa, jipe adhabu wewe unayetofautiana nao, jipe adhabu wewe usiye mnafiki na msemakweli. Je, huu nao unaacha alama.”

Mchangiaji mwingine, Abedi Michael amesema: "Hiyo sheria inafanya kazi pale tu ambapo Serikali inakosolewa? Kwa nini viongozi hutumia dini kufanya mambo ya kisiasa? Nadhani ni wakati mwafaka wa kuirekebisha hiyo sheria ili kuwapa uhuru wa kuzungumza watumishi wa Mungu aliye hai.”

Mwananchi. 



Azam FC kukwea kileleni mwa Ligi leo?




Klabu ya soka ya Azam FC leo inatarajia kushuka dimbani dhidi ya Stand United ikisaka alama tatu ili kuizidi Simba SC katika msimamo wa ligi kuu soka Tanzania Bara.

Mchezo huo utapigwa kwenye uwanja wa Azam Complex majira ya saa 1:00 jioni. Azam FC na Stand United zinashuka dimbani kufungua raundi ya 12 ya ligi kuu ambapo mechi zingine zitachezwa kesho na Jumapili.

Azam FC kwasasa ina alama 23 sawa na Simba yenye alama 23 zikitofautiana idadi ya mbao ya kufunga na kufungwa. Endapo Azam FC itashinda leo itafikisha alama 26 na kuongoza ligi huku ikisubiri matokeo ya mechi ya kesho kati ya Ndanda FC na Simba.

Baada ya mchezo wa leo mabingwa hao watetezi wa Kombe la Mapinduzi watasafiri kuelekea Visiwani Zanzibar kwaajili ya michuano ya kombe hilo inayotarajiwa kuanza Januari mwakani. Azam FC ilitwaa kombe hilo Januari mwaka huu kwa kuifunga Simba kwenye mchezo wa fainali.

Jeshi la Polisi laanzisha uchunguzi kwa matapeli wa mtandaoni


Polisi imeanza kuchunguza wanaotapeli wanawake kwa kutumia mitandao huku wengine zaidi wakijitokeza na kukiri kutapeliwa na mzungu aliyetajwa na gazeti hili katika toleo lake la jana.

Aidha Jeshi la Polisi Kitengo cha Viwanja vya Ndege limesema litawafuatilia wafanyakazi wake ambao majina yao yanatumika katika utapeli huo. Katika toleo la jana, gazeti hili lilieleza kuwa kupitia ahadi ya zawadi kubwa ikiwemo fedha na kutekwa kimapenzi kwa njia ya mtandao, mamia ya wanawake wa Jiji la Dar es Salaam wamejikuta wakitapeliwa mamilioni ya fedha na mzungu anayejitambulisha kwa jina la Don Collins raia wa Uingereza.

Hilo lilibainika baada ya gazeti hili kufanya uchunguzi kwa muda wa zaidi ya mwezi mmoja na kuzungumza na wanawake mbalimbali ambao ni waathirika wa utapeli huo, ambao chanzo chake ni uhusiano wa Facebook.

Matapeli walio katika mtandao wa mzungu Collins huwafuatilia wanawake kwenye mitandao ya kijamii hasa Facebook ambapo huanza kwa kuwaomba urafiki wa kimapenzi na kisha kupeana namba za simu na ndipo mwanzo wa mawasiliano ya kina yanapoanza na baadaye kutapeliwa.

Kutokana na habari hiyo baadhi ya vituo vya televisheni na redio jana viliisoma habari hiyo katika vipindi vinavyorushwa moja kwa moja (live) ambapo wanawake wengi zaidi walipiga simu na kueleza ama wao wenyewe au rafiki, na ndugu zao nao kutapeliwa.

Miongoni mwa televisheni zilizotoa nafasi kwa wananchi kutoa maoni yao au kueleza kama wamewahi kukumbana na mkasa huo, ni Kituo cha Televisheni cha Channel Ten, ambapo mwendeshaji wa kipindi cha magazeti asubuhi, Mary Edward alisema pia amewahi kukumbana na mkasa huo ingawa alishituka kabla ya kutapeliwa.

“Yaani mimi baada ya kuisoma ile habari ya kwenye gazeti lenu, zilimiminika meseji za wanawake wakilalamika kuibiwa kwa staili kama hiyo, sasa hapo ndiyo nikabainisha kuwa kumbe janga ni kubwa zaidi la wizi kwa kutumia staili hii,” alisema Mary.

Mtangazaji huyo alisema, matapeli wa aina hiyo wengi wao wapo hapa hapa nchini na kuwa mara nyingi huwafuatilia na kuwajua wanawake wanaowavizia ili kuwaibia huku wakitumia mbinu za kuwataka kimapenzi na kuwapa ahadi kemkem.

Akizungumzia sakata hilo, Kamanda wa Polisi Kitengo cha Viwanja vya Ndege nchini, Matanga Mbushi alisema kikosi chake kinafuatilia kiundani wizi unaofanywa na matapeli hao na kuhusisha viwanja vya ndege. Alisema matukio kama hayo yanaathiri taswira ya viwanja vya ndege nchini na kuongeza kuwa matapeli wa aina hiyo wanapaswa kusakwa na kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

Hata hivyo, alitoa mwito kwa wananchi kuwataka waepuke kutuma fedha za malipo ya aina yoyote ile yanayohusiana na viwanja vya ndege kwa njia za mawasiliano ya simu bila ya kuwa na uhakika wa nani wanamtumia. Pia aliweka wazi kuwapo kwa mfumo madhubuti wa ulipwaji wa fedha kwenye viwanja vya ndege, ambao si rahisi kwa matapeli kuutumia. Alisema kwa wananchi ambao wanaambiwa kutuma fedha ili mizigo yao ipitishwe kwa njia zisizokuwa halali katika viwanja vya ndege wanafanya makosa kisheria na ni sawa na kushirikiana na wezi.

“Sasa kama wewe upo Dar es Salaam halafu mtu anataka utume fedha ili mizigo yako iachiwe kwenye Kiwanja wa Ndege wa Julius Nyerere (JNIA) ni kwa nini usije mwenyewe kiwanjani kuona nini cha kufanya. “Sasa unajikuta ukiibiwa fedha nyingi huku mwenyewe ukidhani kuwa unacheza dili ya kupitisha mzigo isivyo halali kiwanjani,” alisema Kamanda Mbushi.

Aliongeza; “hili suala hebu ngoja nilifuatilie kiundani ili kubainisha ni kwa nini kwanza wanatumia majina ambayo yanaendana na wafanyakazi wa ndani ya viwanja vya ndege, ninawashauri matapeli hao kuacha kuchafua hadhi ya viwanja vya ndege kwa kufanyia utapeli wao,” aliongeza.

Msaidizi Mkuu wa Kitengo cha kukabiliana na uhalifu kwa njia ya mtandao, Mwangasa Joshua kupitia gazeti hili aliwataka wanawake au watu wengi ambao wametapeliwa na mtandao huo kufika Polisi ili kutoa taarifa ili waweze kusaidiwa badala ya kuhofia.



Israel kukipa kituo cha treni jina la Trump



Waziri wa uchukuzi nchini Israel,Yisrael Katz ametaka kuchimbwa kwa reli ya chini kwa chini kwenye mji wa zamani wa Jerusalem karibu na ukuta wa Magharibi na kupewa jina la Donald Trump.

Yisrael Katz alisema kuwa anataka kumpa heshima Rais huyo wa Marekani kufuatia uamuzi wake wa kutambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel.

Reli hiyo mpya ya chini na kituo cha treni ni sehemu ya mradi wa reli ya mwendo kasi kutoka Tel Aviv inatarajiwa kuzinduliwa mwaka ujao.

Bw. Katz aliliambia gazeti moja la Israel la Yedioth Ahronoth kuwa kuongezwa kwa reli kutoka Tel Aviv kwenda Jerusalem ndio mradi muhimu zaidi kwa wizara ya uchukuzi.

Jeshi la Polisi laanzisha uchunguzi kwa matapeli wa mtandaoni


Polisi imeanza kuchunguza wanaotapeli wanawake kwa kutumia mitandao huku wengine zaidi wakijitokeza na kukiri kutapeliwa na mzungu aliyetajwa na gazeti hili katika toleo lake la jana.

Aidha Jeshi la Polisi Kitengo cha Viwanja vya Ndege limesema litawafuatilia wafanyakazi wake ambao majina yao yanatumika katika utapeli huo. Katika toleo la jana, gazeti hili lilieleza kuwa kupitia ahadi ya zawadi kubwa ikiwemo fedha na kutekwa kimapenzi kwa njia ya mtandao, mamia ya wanawake wa Jiji la Dar es Salaam wamejikuta wakitapeliwa mamilioni ya fedha na mzungu anayejitambulisha kwa jina la Don Collins raia wa Uingereza.

Hilo lilibainika baada ya gazeti hili kufanya uchunguzi kwa muda wa zaidi ya mwezi mmoja na kuzungumza na wanawake mbalimbali ambao ni waathirika wa utapeli huo, ambao chanzo chake ni uhusiano wa Facebook.

Matapeli walio katika mtandao wa mzungu Collins huwafuatilia wanawake kwenye mitandao ya kijamii hasa Facebook ambapo huanza kwa kuwaomba urafiki wa kimapenzi na kisha kupeana namba za simu na ndipo mwanzo wa mawasiliano ya kina yanapoanza na baadaye kutapeliwa.

Kutokana na habari hiyo baadhi ya vituo vya televisheni na redio jana viliisoma habari hiyo katika vipindi vinavyorushwa moja kwa moja (live) ambapo wanawake wengi zaidi walipiga simu na kueleza ama wao wenyewe au rafiki, na ndugu zao nao kutapeliwa.

Miongoni mwa televisheni zilizotoa nafasi kwa wananchi kutoa maoni yao au kueleza kama wamewahi kukumbana na mkasa huo, ni Kituo cha Televisheni cha Channel Ten, ambapo mwendeshaji wa kipindi cha magazeti asubuhi, Mary Edward alisema pia amewahi kukumbana na mkasa huo ingawa alishituka kabla ya kutapeliwa.

“Yaani mimi baada ya kuisoma ile habari ya kwenye gazeti lenu, zilimiminika meseji za wanawake wakilalamika kuibiwa kwa staili kama hiyo, sasa hapo ndiyo nikabainisha kuwa kumbe janga ni kubwa zaidi la wizi kwa kutumia staili hii,” alisema Mary.

Mtangazaji huyo alisema, matapeli wa aina hiyo wengi wao wapo hapa hapa nchini na kuwa mara nyingi huwafuatilia na kuwajua wanawake wanaowavizia ili kuwaibia huku wakitumia mbinu za kuwataka kimapenzi na kuwapa ahadi kemkem.

Akizungumzia sakata hilo, Kamanda wa Polisi Kitengo cha Viwanja vya Ndege nchini, Matanga Mbushi alisema kikosi chake kinafuatilia kiundani wizi unaofanywa na matapeli hao na kuhusisha viwanja vya ndege. Alisema matukio kama hayo yanaathiri taswira ya viwanja vya ndege nchini na kuongeza kuwa matapeli wa aina hiyo wanapaswa kusakwa na kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

Hata hivyo, alitoa mwito kwa wananchi kuwataka waepuke kutuma fedha za malipo ya aina yoyote ile yanayohusiana na viwanja vya ndege kwa njia za mawasiliano ya simu bila ya kuwa na uhakika wa nani wanamtumia. Pia aliweka wazi kuwapo kwa mfumo madhubuti wa ulipwaji wa fedha kwenye viwanja vya ndege, ambao si rahisi kwa matapeli kuutumia. Alisema kwa wananchi ambao wanaambiwa kutuma fedha ili mizigo yao ipitishwe kwa njia zisizokuwa halali katika viwanja vya ndege wanafanya makosa kisheria na ni sawa na kushirikiana na wezi.

“Sasa kama wewe upo Dar es Salaam halafu mtu anataka utume fedha ili mizigo yako iachiwe kwenye Kiwanja wa Ndege wa Julius Nyerere (JNIA) ni kwa nini usije mwenyewe kiwanjani kuona nini cha kufanya. “Sasa unajikuta ukiibiwa fedha nyingi huku mwenyewe ukidhani kuwa unacheza dili ya kupitisha mzigo isivyo halali kiwanjani,” alisema Kamanda Mbushi.

Aliongeza; “hili suala hebu ngoja nilifuatilie kiundani ili kubainisha ni kwa nini kwanza wanatumia majina ambayo yanaendana na wafanyakazi wa ndani ya viwanja vya ndege, ninawashauri matapeli hao kuacha kuchafua hadhi ya viwanja vya ndege kwa kufanyia utapeli wao,” aliongeza.

Msaidizi Mkuu wa Kitengo cha kukabiliana na uhalifu kwa njia ya mtandao, Mwangasa Joshua kupitia gazeti hili aliwataka wanawake au watu wengi ambao wametapeliwa na mtandao huo kufika Polisi ili kutoa taarifa ili waweze kusaidiwa badala ya kuhofia.



Israel kukipa kituo cha treni jina la Trump


Waziri wa uchukuzi nchini Israel,Yisrael Katz ametaka kuchimbwa kwa reli ya chini kwa chini kwenye mji wa zamani wa Jerusalem karibu na ukuta wa Magharibi na kupewa jina la Donald Trump.

Yisrael Katz alisema kuwa anataka kumpa heshima Rais huyo wa Marekani kufuatia uamuzi wake wa kutambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel.

Reli hiyo mpya ya chini na kituo cha treni ni sehemu ya mradi wa reli ya mwendo kasi kutoka Tel Aviv inatarajiwa kuzinduliwa mwaka ujao.

Bw. Katz aliliambia gazeti moja la Israel la Yedioth Ahronoth kuwa kuongezwa kwa reli kutoka Tel Aviv kwenda Jerusalem ndio mradi muhimu zaidi kwa wizara ya uchukuzi.



Omog apata dili la kuinoa El-Merreikh





Siku chache baada ya kufungashiwa virago na Klabu ya Simba, aliyekuwa kocha mkuu wa timu hiyo, Joseph Omog amepata dili nchini Sudan.

Omog ambaye hivi karibuni alifungashiwa virago na Simba kutokana na kushindwa kuiongoza timu hiyo kupata matokeo mazuri katika mchezo wa Kombe la FA dhidi ya Green Warriors amepata dili katika Klabu ya Al-Merreikh ambayo ni moja kati ya miamba ya soka nchini Sudan.

Juzi Jumatano, Al-Merreikh ilimtumia barua pepe Omog ya kumtaka akajiunge na timu hiyo kutokana na kuvutiwa na utendaji wake wa kazi wakati alipokuwa akiitumikia Simba lakini pia wasifu wake alionao katika soka la Afrika.

Habari za kuaminika zinaeleza inadaiwa kuwa baada ya barua hiyo Omog aliwajibu na kuwataka wampatie muda wa mwezi mmoja ili aweze kwenda kwao Cameroon na kuweka mambo yake sawa.

“Omog anatarajia kuondoka nchini Jumamosi endapo atamalizana na uongozi, lakini jana (juzi) amepokea barua pepe kutoka Sudan katika Klabu ya Al-Merreikh ikimhitaji akawe kocha mkuu wa timu hiyo.

“Hata hivyo, aliijibu barua hiyo na kuwaambia wampatie muda kwanza aende kwao akaweke mambo yake sawa,” kilisema chanzo hicho cha habari na kuongeza:

“Pia ukiachana na dili hilo, huko kwao nao wamemuita ili akakabidhiwe majukumu katika timu yao ya taifa kwa ajili ya michuano ya AFCON ya mwaka 2019.

Yanga yatua Mwanza Salama, kuivaa Mbao FC



Kikosi cha Yanga kimetua salama Mjini Mwanza tayari kwa pambano lake la Jumapili dhidi ya wenyeji Mbao FC, pambano la Ligi Kuu ambalo limepangwa kupigwa uwanja wa CCM Kirumba.

Kocha msaidizi wa timu hiyo Shadrack Nsajigwa amesema, timu imewasili salama na leo wanatarajia kufanya mazoezi kwenye uwanja wa Kirumba, pamoja na kesho kabla ya kujiandaa na mchezo huo ambao wameupa umuhimu mkubwa.

“Nashukuru tumewasili salama Mwanza, hali ya hewa ni nzuri na kufika mapema siku mbili kabla ya mchezo kutatusaidia kufanya vizuri kwenye mchezo wetu wa keshokutwa kwasababu tumedhamiria kushinda mchezo huo ukizingatia Mbao ni timu nzuri na imeuwa ikitusumbua sana,” amesema Nsajigwa.

Kocha huyo amesema ukitoa wachezaji Ibrahim Ajibu na Obrey Chirwa wachezaji wote waliobaki na kusafiri na timu hiyo niwazima na wapo katika ari kubwa ya kuhakikisha wanacheza na kuhakikisha wanapata pointi tatu.

Yanga inashika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, ikiwa na pointi 21, huku mahasimu wao Simba wakiwa ndiyo vinara wa ligi hiyo wakiwa na pointi 23 huku Azam FC wakishika nafasi ya pili wakiwa na pointi sawa na Simba.


VIDEO: Rais Magufuli amwagiwa sifa na Sheikh Kishki



Mhadhiri wa Kimataifa wa Kiislamu, Sheikh Nurdeen Kishki amemmwagia sifa Rais wa DK John Magufuli kutokana na uamuzi wake wa kupiga vita uvaaji wa nguo zisizo na maadili katika video za muziki nchini.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI..USISAHAU KUSUBSCRIBE



VIDEO: KAKOBE Aendelea Kupeta Mtaani





Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amefunguka na kusema kuwa jeshi la polisi mpaka sasa halijamkamata Askofu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Zakaria Kakobe kama baadhi ya taarifa zinavyosamabazwa.

Kamanda Mambosasa amesema hayo leo wakati akiongea na waandishi wa habari na kusema kuwa bado hawajamtia nguvuni Askofu huyo na pindi watakapomkamata kwa makosa aliyotenda basi watatoa taarifa hizo.

"Baba Askofu Kakobe bado hatujamkamata pale atakapokuwa amekamatwa kwa makosa aliyotenda nitawaambia lakini kwa sasa hajakamatwa mchungaji huyo, jeshi la polisi huwa halipangi kumkamata mtu bali mtu anapofanya kosa la jinai ndipo anakamatwa hivyo na yeye kama amefanya kosa hili basi tutamkamata" alisisitiza Mambosasa

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI......USISAHAU KUSUBSCRIBE

WHATCH HERE

Auwawa kisa Deni



Mwanaume mmoja mkazi wa Mtaa wa Kilimahewa katika Halmashauri ya mji wa Bunda mkoani Mara, Paul Juma (38), ameuawa kwa kuchomwa mshale wa sumu na rafiki yake, baada ya kutokea ugomvi wa madai kati yao.
Imeelezwa kuwa ugomvi huo ulitokana na Muuaji kudai aongezewe tsh 4,000 kutokana na kumuuzia marehemu mabati manne chakavu kwa tsh 20,000.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mara, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Jafari Mohamed, jana Desemba 28, 2017 alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kumtaja mtuhumiwa kuwa ni Julius Mtoni (48) mkazi wa mjini Bunda na watu hao walikuwa ni marafiki.
Kamanda Mohamed amesema tukio hilo lilitokea mnamo Desema 26, 2017, majira ya mchana wakati watu hao walipokuwa wanakunywa pombe ya kienyeji maeneo jirani na kwa marehemu.
Taarifa kutoka Polisi wilayani Bunda imeeleza kuwa mnamo Desemba 25, 2017 marehemu alimuuzia mtuhumiwa mabati manne chakavu kwa makubaliano ya kila bati tsh 7,000.
Inadaiwa kuwa siku hiyo mtuhumiwa huyo alimpatia marehemu Sh. 20,000 taslimu na kukubaliana kuwa atalipwa kiasi kingine cha Shilingi 8,000 kilichobakia siku nyingine.
Ndipo Desemba 26, 2017 wakiwa wanakunywa pombe, marehemu alimdai mtuhukiwa amlipe Sh. 8,000 zilizokuwa zimesalia, lakini alimpatia Sh. 4,000 na ndio wakaanza kuzozana huku marehemu akishinikiza alipwe deni lake lote la tsh 8,000/=.
Polisi wamesema kutokana na kutokuelewana, marehemu alianza kumkaba mtuhumiwa, ndipo mtuhumiwa akakimbilia nyumbani kwake na kuchukua upinde na kumfyatulia mshale ambao ulimpata begani.
Polisi walisema kuwa baada ya marehemu kuchomwa mshale huo aliuvunja na kubakiza kipande cha mshale huo mwilini mwake na kukimbilia polisi, lakini alipoteza maisha kutokana na kutokwa na damu nyingi.